Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mungano na Mazingira kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mungano na Mazingira kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nashukuru. Nina mambo mawili tu ambayo napenda kuchangia. Kwanza, nimpongeze Mheshimiwa Makamba kwa kazi kubwa anayoifanya, tumemuona maeneo mbalimbali hasa maeneo ya mazingira na kule Zanzibar kutatua matatizo mbalimbali. Hata hivyo, kuna mambo ambayo nadhani juhudi zinazofanyika haziendani na matokeo yatakavyokuja kuwa. Na mimi nina mambo mawili tu ambayo nataka kuchangia kwa dakika hizi tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza ni la Zanzibar, bidhaa kutoka Zanzibar kuingia katika soko la Tanzania Bara (soko la Tanganyika). Nimeona kwenye taarifa ambayo Waziri amezungumza, amesema kwamba miongoni mwa majukumu anayoyafanya ni kuondoa vikwazo vya biashara kati ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Kamati imempongeza Waziri na Ofisi ya Makamu wa Rais, kwa kuzikutanisha sekta za biashara za pande mbili za Muungano kwa ajili ya kujadili upatikanaji wa fursa za masoko kwa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Mheshimiwa Waziri anafahamu kwamba katika stages za integration sisi tuko stage ya juu kabisa ya political federation. Kwa maana ya kwamba tumeshapita kwenye free trade area, customs union, common market, monitory union na sasa tuko kwenye political federation. Iweje leo tuanze kuzungumza kuondoa vikwazo vya biashara wakati katika hali ya kawaida ilitakiwa bidhaa zote zinazozalishwa Zanzibar ziingie kwenye soko la Bara bila vikwazo vya aina yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo mengi ya Muungano yanasababishwa na Tanzania Bara kuzuia fursa za kiuchumi za Zanzibar. Leo hii Serikali inasema kwamba, inazuia kwa mfano, sukari kutoka Zanzibar kwa sababu ya kuzuia magendo, lakini hii hii Tanzania Bara ambayo inazalisha sukari Kagera na bado ina-import sukari kutoka nje, inaruhusu Kagera kuuza sukari Uganda. Kuna sukari kutoka Mumias Sugar inayoingia huku Tanzania Bara kwa sababu tupo kwenye East African Common Market, bidhaa zinatembea bila vikwazo vya aina yoyote, iweje Zanzibar izuiwe kuleta bidhaa zake huku? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ni suala la udhibiti wa bidhaa ambazo zinatoka nje wanasema kwamba sijui kuna sukari kutoka Brazil na kadhalika kwenye customs union kuna kitu kinaitwa rules of origin. Kwa hiyo, wataalam na maafisa wa Wizara ya Viwanda na Biashara wangekuwa kule Zanzibar wakatazama kinachozalishwa, wakatoa rules of origin bidhaa hii ikaingia huku kuuzwa.

Kwa hiyo, inavyoonesha hapa ni dhahiri kwamba uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano sasa hivi hauna nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba Zanzibar inajitegemea kiuchumi ili Tanzania Bara iendelee kuitawala Zanzibar kiuchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa naomba jambo hili liweze kupatiwa ufumbuzi kwa sababu hakuna sababu yoyote ile ya kuzuia bidhaa yoyote kutoka Zanzibar kuingia Tanzania Bara kwa sababu sisi…

T A A R I F A . . .

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni mazingira. Nafahamu kwamba sasa hivi tunashughulika na Stiglers’ Gorge na kadhalika, lakini tunafahamu kwamba kuna madhara makubwa sana ya mradi huu. Kwa sababu Waziri amesema wamefanya tathmini wanayo ofisini, tunaomba Bunge lipate tathmini ambayo Wizara imefanya kuhusiana na mradi wa Stiglers’ Gorge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, muhimu zaidi ni kwamba, kuna miradi mingi sana iliyoainishwa kwenye Power System Master Plan ambayo ingeweza kuzalisha umeme sawasawa na huo umeme ambao tunaenda kuuzalisha Stiglers’ Gorge. Serikali haitekelezi miradi hiyo, inaamua kuingiza fedha za umma, tena tunajitamba kwamba tutatengeneza kwa fedha zetu za ndani, tunaenda kupoteza fedha nyingine kwenye mradi ambao utakuwa white elephant. Kwa sababu Stiglers’ Gorge iko down stream, kuna miradi ambayo ilipangwa ipo up stream ambayo ingeweza kuzalisha umeme huohuo ambao tunataka kuuzalisha kwenye Stiglers’ Gorge.