Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni zamu yangu na mimi kuweza kuchangia kwenye Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze na hoja ya kwanza ambayo ni walimu wa shule za sekondari kuhamishiwa shule za msingi bila kupewa haki zao kisheria.

Mjeshimiwa Mwenyekiti, hata kwenye kitabu hiki cha hotuba ya Waziri wa TAMISEMI ukiangalia ukurasa wa 40 wameeleza pale kwamba walimu 8,834 walihamishwa kutoka shule za sekondari kupelekwa shule za msingi ili kupunguza tatizo la walimu shule za msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza kabisa, kumtoa mwalimu kutoka shule ya sekondari kwenda shule ya msingi hii si sahihi hata kidogo. Kwa sababu huyu mwalimu amejifuza saikolojia ya kufundisha watoto wa sekondari wenye umri mkubwa kuliko wale wa shule ya msingi, leo unapomtoa sekondari kumpeleka shule ya msingi tunakwenda ku-prove failure na hauwezei kupata efficiency hata kidogo na matokeo yatakuwa ni mabaya kweli kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huku ni kukwepa majukumu, Serikali inafika mahali inakwepa majukumu, badala ya kuajiri inafika mahali inaanza kuhamisha walimu wa sekondari kupeleka shule za msingi. Mheshimiwa Waziri, naomba nikuhakikishie kwamba huko sekondari mnakosema walimu wanatosha, sekondari, walimu hawatoshi kwasababau unavyozidi kuongeza idadi huku shule za msingi hata kule sekondari idadi ya wanafunzi inakuwani kubwa sana. Kwa hiyo, mnachokifanya Mheshimiwa Waziri kabisa hamuwatendei Watanzania haki hata kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo lakini bado walimu hawa 8,834 wamehamishwa, lakini hawajalipwa fedha zao. Hawajalipwa disturbance allowance, subsistence allowance, wala transport allowance.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi walimu 117 waliohamishwa kutoka shule za sekondari kwenda shule za msingi wanadai zaidi ya shilingi milioni 300 hawajalipwa hadi leo. Serikali hii ambayo inasema ni Serikali ya wanyonge, wanyonge gani ambao hawajalipwa mpaka leo? Wanyonge ni akina nani kama leo walimu 117 wanadai shilingi milioni 300 na kitu hawajalipwa? Huyu anayejiita kiongozi wa wanyonge ni wanyonge wapi? Hii hali ni mbaya sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi juzi mmefuatilia maandamano yamefanyika kule Mbozi na walimu hawa 117, Rungwe walimu zaidi ya 80 wameandamana wanadai fedha hazijalipwa. Waziri wa TAMISEMI uko hapo, ukweli ni kwamba Waziri wa TAMISEMI katika hili mme-prove failure kabisa na mlishaizungumzia siku za nyuma wkamba watumishi wasihamishwe bila kulipwa lakini leo mmeshindwa kufayakazi hiyo ya kuwalipa hawa watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niende kwenye suala lingine la ajira za watumishi. Leo Serikali inakwepa kuajiri watumishi, Awamu hii ya Tano haiajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe mfano mdogo tu, ukisoma ukurasa wa 40 wa hotuba hii ya Waziri wa TAMISEMI wanasema, katika mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali imefanikiwa kuajiri walimu wapya 2,767. Unapoajiri walimu 2,767 wakati kwenye ukurasa huo huo tumeambiwa kwamba upungufu wa walimu kwenye shule za msingi ni walimu 97,517 unaajiri 2,767 tafsiri yake ni kwamba kama tutakuwa hatuzaliani unahitaji miaka 35 ili kuweza kumaliza tatizo la walimu shule za msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii Serikali ya Awamu ya Tano ukilinganisha na awamu nyingine ndiyo Serikali ambayo naona mimi ime-prove failure hamna kilichofanyika kabisa imeshindwa bora hata Serikali ya Jakaya Mrisho Kikwete tunaikumbuka kuna mambo alifanya mazuri, lakini hii ya wanyonge sidhani ni wanyonge gani anaozungumzia

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kufuta, lakini nasema ujumbe hapa ni kwamba Awamu ya Tano haijaajiri, haitoi ajira.

Kwa hiyo, ukichukua hawa walimu, ukichukua miaka 35 tafsiri yake ni kwamba kama Watanzania hatuongezeki, kwa maana hatuzaliani kuanzia leo tunahitaji kuwa na miaka 35 mingine mbele. Ukijumlisha leo ni mwaka 2018 maana yake ni mwaka 2053 ndipo tatizo la walimu litakuwa limekwisha nchini. Kwa muda huo sidhani kama sisi tutakuwepo kwa sababu kutakuwa na chama kingine kinanachoongoza nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lingine ni mishara kwa watumishi wa umma. Mishahara haiongezwi, Awamu hii ya Tano haijawahi kuongeza mshahara hata mara moja. Gharama za maisha zinapanda, hali ya uchumi inazidi kuwa mbaya, leo watumishi wanapokuwa wanajaza mikataba wanaanza kazi maana yake pale, pamoja na mikataba yao ni kwamba wanasaini kwamba watakuwa wanaongezewa mshahara annual increment kila mwaka, watakuwa wanaongezewa mishahara, wakipandishwa mishahara. Leo hawapandishwi madaraja, hawajaongezwa mishahara ndiyo awamu pekee ambayo haijawahi kuongeza mishahara, na ndiyo Serikali ambayo inajiita Serikali ya wanyonge, sijui wanyonge wapi hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongeze jambo lingine, shilingi milioni 50 za kila kijiji. Usiku wa deni haukawii kuisha; na mimi nawakumbusha amezungumza Mheshimiwa Heche vizuri sana asubuhi. Usiku wa deni ni mwaka kesho kutwa 2020. Kwanza kuanzia mwakani Serikali za Mitaa tutakwenda kuwakumbusha Watanzania shilingi milioni 50 mlizowaahidi hadi leo hamjatoa na muda unazidi kuisha. Kwa hiyo ndugu yangu Mheshimiwa Jafo, Waziri wa TAMISEMI utatuambia hizi shilingi milioni 50 kwenye bajeti hii zipo au hazipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni suala la ubaguzi wa Watanzania. Kuna watu wanaohojiwa uraia wao, viongozi wa dini maaskofu, Askofu Kakobe, Askofu mmoja anaitwa Severine Niwemugizi wa Kanisa la RC hawa watu pamoja na viongozi wengine mbalimbali, wanafunzi Abdul Nondo. Watu leo hii wameanza kubaguliwa uraia wao, wanahojiwa uraia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inafika mahali kama yule askofu kule Bukoba anasema kwamba kiongozi akatubu, tunataka Katiba mpya. Mtu anapotoa maoni yake ambayo amepewa uhuru wa maoni na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unakwenda kumhoji uraia, kwa nini kabla hajatoa maoni yake msingemhoji uraia? Kiongozi asiyekubali kukosolewa hawezi kuwa kiongozi, lindeni uhuru wa maoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amezungumza ndugu yangu Zitto Zuberi Kabwe, mkitaka basi Mkoa wa Kigoma kama kuna uwezekano basi upelekeni Burundi. Kwa sababu leo inaonekana tatizo kubwa la kuhoji uraia wa watu mnahoji sana watu wa Kigoma. Abdul Nondo mwanafunzi wa chuo kikuu ni mtu wa Kigoma, Askofu Kakobe ni mtu wa Kigoma, wako na wengine n mifano mingine. Leo kukaa mipakani imekuwa ni dhambi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na wewe mimi naamini kama unakaa karibu na mpakani kule si ajabu ukaja kutoa ushauri wako au maoni yako watakuja kukuhoji sijui uko jirani na nchi gani. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee. Wanasema wamba kama umezoea kula nyama ya binadamu huwezi kuacha, ndugu yangu Hussein Bashe amewahi kuhojiwa uraia wake eti kwa sababu kaingia kwenye kura za maoni na ndugu yangu huyu Waziri wa Maliasili amehojiwa akaambiwa si raia wa Tanzania.

Leo dhambi hiyo ya kuhoji watu haijaisha, kuwabugua watu kura za maoni zimekwisha leo Bashe amekuwa raia wa Tanzania ni kwa sababau kura za maoni zimekwisha na leo ni Mbunge mwenzetu kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kumbe hiyo tabia haikwisha imeendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali hii ni mbaya sana na tunaomba tuikemee kwa pamoja sisi wote kwa sababu leo hii kwa kuwa mtu mwingine, kwa Kakobe leo imetokea kwa Bashe na kwa wengine imetokea kwa Nondo kesho na kesho kutwa ni dhamu yako, kwa kumalizia naomba nizungumze suala… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)