Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipatia fursa ya kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Nitachangia kwa kujaribu kujibu hoja za Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu, niwapongeze Waheshimiwa Mawaziri wenzangu walio katika Ofisi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu na watendaji wote wa Wizara hii ambayo kimsingi ni Wizara ya uratibu. Sisi ili tuweze kufanya kazi zetu tunawategemea sana, ahsanteni kwa msaada mnaotupa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mambo mengi yaliyozungumzwa, niwashukuru Waheshimiwa Wabunge, yananijengea uwezo wa kuwaletea hotuba nzuri ambayo italenga kujibu matakwa yenu. Hata hivyo kuna mambo ambayo ningeomba niyajibu leo kusudi niweze kuchangia vizuri Hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la msingi la kwanza ni suala la viwanda. Kuna kutoelewa au tuna kuelewa tofauti juu ya suala la viwanda. Ukisoma Mpango wa Pili wa Miaka Mitano tumeamua kujenga uchumi wa viwanda na dhima yetu ni ujenzi wa uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya watu. Mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya watu ndiyo center.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunalenga ifikapo mwaka 2025 hii iwe nchi ya uchumi wa kati kwa kupitia uchumi wa viwanda. Sasa Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote ili tujenge uchumi wa viwanda kwa mtu ambaye alikuwa hajui viwanda lazima kulingana na matabaka yetu na uwezo wetu twende kwenye makundi manne ya viwanda. Mimi kiwanda ninachokiita kidogo mwenzangu atakiita kikubwa ndiyo maana tunahimiza falsafa ya viwanda vidogo sana, viwanda vidogo, viwanda vya kati na viwanda vikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwatie shime Watanzania na tuwaangalie waliotutangulia. Nchi ya India ambayo yenyewe ina population ya bilioni 1.256 lakini ina income per capita ya dola 1,800 unaweza kuzidisha ukapata GDP yake. Asilimia 38 yake inatokana na viwanda vidogo. Bidhaa unazozikuta madukani India asilimia 40 inatokana na viwanda vidogo, lakini mauzo ya India nje asilimia 45 inatokana na viwanda vidogo. Sasa ukisoma andiko la Mchungaji Profesa Adam Persia anakueleza kwa nini viwanda vidogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda vidogo hasa kwetu Watanzania ni shule, kama hujawahi kumiliki kiwanda, usianze na kiwanda cha bilioni mia tano, anza na kiwanda kidogo. Kiwanda kidogo kinakufaa wewe muanzishaji, lakini ni shule una-train family, ndiyo maana; napenda niliseme hili; ndiyo maana unakuta family za wenzetu kama Madhvani mimi nimezaliwa nasikia Madhvani mikaa 65 iliyopita Madhvani alikuwepo Uganda, lakini Madhvani mpaka leo yupo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana mkagundua sisi Wabunge, Watanzania wote kwa nini tunasoma na watoto wa Wahindi mashuleni lakini hatuombi kazi pamoja na wao? Ni kwa sababu wanakuwa trained kwenye family business na wanaweza kuendelea miaka mingi na mingi. Kwa hiyo nawasihi muwe mashuhuda, campaigner, mhimize Watanzania wakubali suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapozungumza suala hilo tunakwenda kwenye jibu la viwanda, tuna viwanda vingapi? Nina rafiki yangu mmoja Mbunge wa Monduli anasema viko wapi? Hivyo viwanda 3,306 vipo na viko Tanzania. Nimekwenda kutafuta takwimu za viwanda vile, viwanda tulivyonavyo Tanzania ni zaidi ya viwanda 53,000, vimechapwa kwenye karatasi za A4 karatasi 900. Kwa hiyo vipo, vipo Tanzania na ukiviangalia kila kijiji kina kiwanda kimeorodheshwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivyo viwanda vinafanya kazi gani? Tumeelekezwa kwamba tuanzishe viwanda ambavyo vitachakata mazao ya shamba, mazao tunayoyalima sisi. Faida ya viwanda hivi hata kama ni vidogo vinaongeza life span ya product na vinapunguza post-harvest loss, ndiyo maana ya kuhimiza hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwape mfano mmoja tulionao sasa hivi wa watu wa Dodoma. Dodoma wana zabibu, sasa hivi zabibu inapata tatizo la soko kwa sababu ya mambo fulani ambayo tunayarekebisha, lakini mtu mwenye kiwanda kidogo cha shilingi 500,000 au 600,000 unaweza kuchukua zabibu ukasaga, unapata mchuzi unauweka kwenye gudulia ambapo unasubiri wakati soko likipatikana unaweza kuuza. Mheshimiwa rafiki yangu ambaye ni mkulima wa zabibu anaelewa kitu hicho. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nawasihi toka hapa kabla ya andiko langu halijaja muweze kuhubiri viwanda vidogo. Niwaahidi, nimeandika kitabu kuhusu viwanda vidogo nitakitoa kabla ya bajeti yangu, lakini na bajeti inayokuja ni kitabu cha rejea. Kama hujui viwanda ukisoma bajeti yangu nitakayoiandika utaweza kuelewa suala la viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie mazingira ya biashara. Wengi wamezungumzia mazingira ya biashara. Mimi narudia kauli ya viongozi wangu; Mheshimiwa Rais amelizungumzia, Mheshimiwa Makamu wa Rais amelizungumzia, Mheshimiwa Waziri Mkuu amelizungumzia suala la mazingira ya biashara. Zaidi tumeandika andiko (regulatory reform) ambayo inaitwa almaarufu blue print; tunataka hivi vikwazo viondoke. Hata hivyo ukisoma maandiko hii kazi haikuanza leo. Mpango wa kwanza wa miaka mitano ilikuwa kuondoa vikazo, haikumalizika, tumekwenda nayo na hivi vikwazo vitaondoka na nyingine tusilaumiane ni mind-set. Kuna mtu ukiingia ofisini amezoea kuwanunia watu sasa hilo sio tatizo la Waziri wake au Katibu Mkuu wake ndivyo alivyo na tutawabadilisha hao watu waweze kufanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala la viwanda limezungumziwa suala la matrekta ya URSUS au matrekta yaliyoko TAMCO almaarufu kama alivyokuwa akiyaita ndugu yangu Dkt. Mwigulu Nchemba kwamba ni matrekta ambayo yana lengo la kuondoa jembe shambani kulibakiza kwenye ile bendera ya chama anachokipenda na makaburini kusawazisha makaburi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge kwa nini matrekta ya URSUS hayajauzwa, yana maelekezo maalum, Mheshimiwa Waziri Mkuu ameelekeza yale matrekta yaende kijijini sasa huyo mtu wa kijijini unampaje? Tunatengeneza utaratibu tukishirikiana na Hazina kwamba Wabunge mpewe, wafanyakazi mpewe na ma-DC wapewe yaende vijijini si matrektra ya kuvuta mizigo. Watu walileta matrekta unayakuta airport, au unayakuta bandarini, haya yanakwenda vijijini. Tuna matrekta 2,400 kwa hiyo Waheshimiwa Wabunge, yakija myagombanie kama mpira wa kona myapeleke vijijini, halafu mtaona mwaka 2020 mambo yatakavyokuwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie miradi ya kimkakati. Miradi ya kimkakati inatekelezwa, mnaweza mkawa mnaona uchelewesho, wengine mnasema twende haraka, lakini sheria tuliyoitunga sisi Wabunge mwaka jana ya kuangalia maslahi ya Taifa imetufanya ile mikataba kwa mfano ya Mchuchuma na Liganga iangaliwe mara tatu au nne.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwaeleze, mimi nilikuwepo; nilimsikia Rais wa Zambia na wengi mmeona clip za Zambia na kuna nchi nyingine wanalia, waliingia mikataba unakuta kila kitu kimechukuliwa. Naogopa na namkumbuka kaka yangu ambaye alikuwa Waziri hapa. Aliwahi kusema mtafanya maamuzi, maamuzi hayo hata kama mmekufa makaburi yenu yatafungwa minyororo ndivyo alivyosema Sebastian Rweikiza Kinyondo. Nisingependa mimi kaburi langu lifungwe mnyororo.

Kwa hiyo, hii miradi ya kimkakati tusingependa kufanya maamuzi, kwa hiyo tunaipitia na tunapoipitia tunazungumza na ninyi mje mtuhoji mtuelekeze.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kuwapongeza Wabunge ambao wametupa information where we are getting wrong, lakini kama nilivyowaahidi nitazungumza nanyi zaidi katika bajeti yangu ambayo nimeahidi kitakuwa kitabu cha rejea. Ahsanteni sana naunga mkono hoja.