Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya Waziri Mkuu kuhusu bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019. Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli imedhamiria kwa dhati kujenga uchumi wa kisasa unaoongozwa na falsafa ya uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa na sera msingi ya kuimarisha miundo msingi ya uchumi ikiwemo kujenga reli ya kisasa ya standard gauge, ununuzi wa ndege moja kuongeza uzalishaji wa umeme kwa kuanzisha mchakato wa kujenga bwawa la kuzalisha umeme megawatt 2,100 ili kuunganisha nguvu za uzalishaji umeme kwa kutumia maji na ule wa kutumia nguvu za gesi asilia ili kuwezesha ujenzi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano imefanikiwa kwa kiwango kikubwa pia kuboresha na kuboresha bandari zetu katika mwambao wa bahari ya hindi na zile za maziwa makuu ya Viktoria, Tanganyika na Nyasa. Lengo kuisaidia nchi yetu kuwa kiongozi katika kukuza biashara katika nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze pia Serikali kwa jitihada zinazozifanya za kuboresha huduma za afya kwa Watanzania ambapo vituo vya afya na hospitali nchini zimeboreshwa kwa kuongeza vifaa tiba, madawa na wataalam na matokeo yake vifo vya akinamama na watoto vimepungua kwa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, naiomba Serikali iongeze nguvu katika kukiimarisha kitengo cha kukabiliana na maafa hasa baada ya nchi yetu kuanza kutishiwa na matukio na matishio makubwa ya majanga ya kiasili ambapo siku za karibuni tumeshuhudia matukio ya matetemeko ya ardhi yametikisa maeneo ya nchi yetu hasa katika kanda ya ziwa Mkoani Kagera na hata tarehe 25 Machi, 2018, Kata za Ngemo na Ushirika zilipatwa na janga la kupigwa na tetemeko la ardhi ambapo madhara katika majengo ya Taasisi za Umma na watu binafsi yaliathiriwa vibaya na watu kujeruhiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitengo cha kuratibu na kukabiliana na maafa kiimarishwe maana kutokana na mabadiliko ya tabianchi tumeanza kuona vimbunga kutokea baharini vikianza kulikaribia bara la Afrika ikiwemo nchi yetu kuhusiana na vita dhidi ya madawa ya kulenya. Naipongeza Serikali kwa namna inavyokabiliana na janga hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, naishauri Serikali kuongeza jitihada za kusambaza dawa za kutibu waathirika wa dawa za kulevya yaani methadone dawa hizi ziweze kupatikana katika Wilaya nchini. Naipongeza sana Serikali kwa jitihada zake za kutupatia fedha shilingi milioni 800 kwa ajili ya upanuzi wa vituo vya afya viwili vya Iboya na Masumbwa ambapo ujenzi unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, naishukuru sana Serikali kwa jitihada zake za kuanza ujenzi wa hospitali ya Wilaya na ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe pamoja na Ofisi na Makazi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya Waziri Mkuu.