Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wanyama waharibifu. Serikali iwe na mikakati ya wazi katika kuzuia wanyama waharibifu katika Vijiji vya Hunyari, Kisambu Nyangere, Mariwanda, Sarakwa, Mugeta Kyandege na Tingirima. Maeneo haya kwa muda mrefu yameathirika sana kwa wanyama kula mazao yao ya chakula na biashara toka msimu wa 2011/2012 hadi leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu fidia ya kifuta jasho. Tunaomba Serikali kulipa fidia ya kifuta jasho na kifuta machozi zaidi ya shilingi milioni 360 zinadaiwa na wakulima wa Vijiji vya Nyangere, Mariwanda, Kihumbu, Sarakwa, Tingirima, Mugeta na Sarakwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, msaada wa kumalizia majengo matatu ya zahanati, kuna maeneo yaliyo mbali na huduma za afya, wakazi wa vijiji husika wamejenga zahanati ili kusaidia kupata huduma za afya. Majengo matatu yameezekwa bado samani, lipu, floor, nyumba ya Mganga katika Vijiji vya Tiring’ati, Kambubu na Mihingo. Tunaomba Serikali kusaidia vijiji hivi ambavyo vipo mbali na huduma ya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu miradi ya maji katika Jimbo langu kuna uhaba mkubwa wa maji ya binadamu na mifugo na hapa ieleweke kuwa katika vyanzo vya maji katika Jimbo langu maji ya malambo na mabwawa ndio maji ya binadamu na mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Serikali kukarabati malambo ya zamani ya Kyandege, Mugeta, Tingirima, Nyang’aranga, Manchim, Wero, Mahanga, Salama A, Sarzate, Rakanaa, Mihingo, Mekomariro (Malambo mawili) na Sarakwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, malambo haya yalipangwa kuchimbwa sana budget ya 2016/2017 hadi leo hakuna dalili, Mheshimiwa Waziri wa Maji aliahidi humu Bungeni, Bunge la Mwezi wa Pili, 2018 na kwamba Bunda imetengewa bilioni moja kwa kazi hiyo. Malambo yanatumika zaidi kwa maji ya binadamu kwa visima kukauka kila kiangazi. Suala la Malambo katika Jimbo langu yana umuhimu zaidi kuliko visima, maana visima hukauka kila kiangazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Kitengo cha SENEPA wamekubali kutoa vifaa na ufundi kusaidia kukarabati malambo haya, tunaomba Serikali ikubali kusaidiana na Wizara ya Maji kukarabati malambo haya yaliyochimbwa miaka ya 60 lakini ni chanzo cha uhakika cha maji katika jimbo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.