Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DKT. HAJDI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya uzalishaji (kilimo); Serikali ilichukua mkopo wa Dola za Kimarekani milioni 40 kwa kununua na kusambaza matrekta na zana zake mwaka 2010. Hadi ilipofika mwaka 2015 ni asilimia 46 tu madeni ya mauzo ya matrekta hayo yalikusanywa. Mradi huu umekumbwa na changamoto nyingi pamoja na SUMA JKT kukosa uzoefu katika masuala ya biashara hivyo kusababisha mradi huo kuwa na hasara kubwa kwa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipindi kifupi sana kimepita katika mradi huu wa SUMA JKT wa matrekta kuonesha hasara, Serikali 2017 imechukua mkopo mwingine wa matrekta ya aina ya Ursus yanaunganishwa na kampuni ya Kibaha chini ya NDC. Watekelezaji wa mradi huu wa matrekta ya Ursus wanaonesha toka Mwanza na hawana uzoefu kabisa katika masuala ya biashara ya matrekta na zana za kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali itoe maelezo na kutuhakikishia Watanzania kwanza fedha zetu za SUMA JKT, tractors zitarudishwa au tayari tumeshapata hasara. Pili; nashauri Serikali kuwawezesha NDC wajiendeshe kibiashara katika kutekeleza mradi wa Ursus tractors pamoja na kutumia mikakati/mbinu zote za masoko yaani marketing strategies za (1) Promotion (2)Price (3) Place (4) Production vinginevyo nao Ursus tractors project unaweza ukaishia hasara kama ule wa SUMA JKT (tractors project)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.