Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, marejesho ya mkopo; suala la fedha zinazotengwa asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri hukopeshwa vijana na akinamama. Fedha hizo zinaporudishwa hazifuatiliwi na nyingi hutumika katika mafungu mengine katika halmashauri husika. Wabunge tumekuwa tukidai zitolewe lakini hatudai marejesho ya mikopo hiyo. Namwomba Mheshimiwa Waziri Mkuu kupitia Waziri anayehusika na Uwezeshaji wa Vijana kutoa maelekezo ya fedha zinazorudishwa na waliokopeshwa ambao ni vijana na akinamama, fedha hizi za marejesho hazisimamiwi kikamilifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu na Waziri wa Nchi katika utekelezaji uliotukuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.