Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. NURU AWADHI BAFADHILI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya na uwezo wa kuzungumza. Vile vile nimpe pole Mheshimiwa Spika, Mungu azidi kuimarisha afya yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitazungumzia kuhusu barabara zilizo chini ya TARURA. TARURA kwa kweli hadi hivi sasa hawajaeleweka kwa wananchi. TARURA japo inashughulikia barabara lakini bora ingewashirikisha Madiwani. Madiwani ndio wanaozijua barabara zetu zilivyo. Ikiwa TARURA haitawashirikisha Madiwani barabara zetu zitazidi kuharibika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu kauli ya Mheshimiwa Rais Dokta John Pombe Magufuli ya Tanzania ya viwanda. Tanzania ya kuelekea uchumi wa viwanda hiyo ni kaulimbiu nzuri lakini tujiulize, je, umeme wa kuendesha viwanda hivyo upo wa kutosha? Lazima Serikali ihakikishe tunatumia mito tuliyonayo, mfano Mto Rufiji, Kilombero na Mito mingine ambayo ina maji ya kutosha ili izalishe umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umeme tulionao hauwezi kukidhi kuendesha viwanda vinavyohamasishwa vianzishwe.

Kila mkoa umepewa agizo la kujenga viwada 100, je, viwanda hivyo vilijengewa umeme wa kutosha na utapatikana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu atueleze, Je na umeme wa kuendesha viwanda utapatikana bila tatizo?