Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, maendeleo endelevu yanahitaji umoja wa Kitaifa (ushindi ni ushirikiano). Tarehe 21 Februari, 2018, Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) tulifanya mashauriano ya pamoja kati ya Viongozi Wakuu wa Dini na Viongozi Wakuu wa Vyama vya Siasa lengo likiwa kushauriana maudhui yaliyo kwenye lengo la 16 la Malengo Endelevu ya Dunia (Amani, Haki na Ujenzi wa Taasisi Imara). Tulikubaliana kwamba kuna umuhimu wa kuendelea na mashauriano haya kwa kushirikisha Serikali kwa kuwa mapendekezo yetu yameshafikishwa Serikalini, ni vyema mashauriano haya yakafanyika haraka iwezekanavyo kwani kuna viashiria vya wazi vya kuvunjika au kutoweka kwa amani yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, naikumbusha Serikali kwamba dunia ya leo ni meza ya mazungumzo. “Meli ya amani inazama nasi wasafiri tukiwa ndani.”