Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2017/2018

Hon. Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2017/2018

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nianze kwa kuchangia hoja hii kwanza kwa kuunga mkono hoja kwa ujumla. Nianze kwanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi nzuri ambayo anaifanya, lakini bila kusahau kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu ambaye kwa kweli ameonesha ujasiri mkubwa katika kupambana na gurudumu hili la maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu leo itakuwa moja tu kubwa. Tanzania wakati tunawasaidia wenzetu wapigania uhuru wa Nchi za Kusini mwa Afrika tulikuwa na makambi, kuna maeneo ambayo yalikaliwa na wakimbizi kwa nchi yetu zaidi ya maeneo 163, Mheshimiwa
Mwenyekiti, ilikuwa Dar es Salam, Mwanza, Mbeya, Mtwara, Lindi, Ruvuma, Pwani, Iringa, Dodoma, Tabora, Kigoma, Morogoro, Mara, Arusha, Zanzibar na Kagera. Kwa kutunza muda siwezi kuyataja makambi yao yote lakini lengo langu ni moja kwamba Dar es Saalam katika zile Ofisi Ndogo za CCM pale Lumumba baaada ya kuzaliwa Chama cha TANU ilifanywa Ofisi ya wapigania uhuru ambapo Chama cha SWAPO, FRELIMO, ANC, ZANU na POLISARIO walifanya kama makazi pale, kama ofisi zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi za Kamati ya Uongozi ya Afrika (Special Unity) sasa hivi ni ofisi ambazo zinatumiwa na Tume ya Maadili ya Uongozi, makazi ya Hayati Eduardo Mondlane Osterbay, sasa hivi inatumika kama Ubalozi wa Msumbiji; Shule ya Sekondari Makongo na Lugalo walisoma watoto wa wapigania uhuru kwa sasa ni sekondari na Uwanja wa Magunia kule Tandale bado unatumika, ilikuwa ni sehemu ya mkutano pale, walifanyia mikutano pale. Morogoro kambi za wakimbizi zilikuwepo pale, kulikuwa na Mazimbu ambako sasa hivi ni Chuo cha Sokoine, kambi za Dakawa ambako sasa hivi kuna VETA na sehemu nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nia yangu ni kwamba kule Kilolo, Kihesa Mgagao walikaa wakimbizi, naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu tujaribu kubadilisha matumizi, wamefanya magereza ambayo haina tija kwa sababu wafungwa wako 40. Juzi Mheshimiwa Waziri wa Michezo tulipata ugeni kutoka Afrika Kusini kwenda kutembea kwenye kambi ile, alivyosikia kwamba ni magereza alikataa kwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale kuna sehemu ambapo Mheshimiwa Mandela na Sisulu walilala. Tulitegemea sasa kingekuwa ni kivutio kikubwa cha watalii. Kuna watoto pale wameachwa na wenzetu wa South Africa wengi tu. Kuna mambo ya kimsingi kabisa tungeweza kufanya sehemu hii kuwa kivutio kikubwa cha utali tungeweza kuingiza fedha kwenye nchi yetu bila matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali yetu, Mheshimiwa Rais anasikia, Mheshimiwa Waziri Mkuu na timu yake wanasikia wabadilishe matumizi kwa eneo lile ili tufanye aidha shule, chuo au VETA. Sasa hivi tunaenda kwenye nchi ya viwanda tunahitaji kutayarisha vijana wengi ili waweze kufanya shughuli hizo za viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili linawezekana…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.