Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa vile dakika nilizonazo ni chache naomba sasa niende moja kwa moja kwenye kuelezea hali halisi ya kibishara inayoendelea Zanzibar. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi zote zilizoungana na visiwa kama Tanganyika ilivyoungana na Visiwa vya Zanzibar hutumia visiwa hivyo kama strategic center za kibiashara kutokana na geographical position za visiwa. Kwa bahati mbaya sana mpaka sasa Serikali yetu haijaona umuhimu wa kutumia Zanzibar kama center ya kibiashara kwa maslahi ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, miezi michache iliyopita Tanzania Bara ilipatwa na shortage ya sukari ambayo kwa taratibu za Serikali ilizozichukua sina mashaka nazo, hatua ambazo Serikali imechukua ku-solve tatizo hili pia sina mashaka nazo. Mashaka na malalamiko yangu makubwa kwenye hili ni baadhi ya Watendaji wa Serikali kulichukua hili jambo na kulitekeleza kinyume na maagizo ambayo yametokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ambayo inaendelea sasa kwenye bandari yetu, Wazanzibar au wananchi wetu hawana ruhusa hata ya kuingiza sukari kilo mbili kwa ajili ya matumizi yao binafsi. Tatizo hili limekuwa kubwa mpaka sasa wananchi wetu hawawezi kuingiza hata kilo mbili za matumizi yao ya kawaida. Kisa tu tamko lilitoka, kibali hakijatoka na utekelezaji huo umekuwa namna hiyo ambayo naielezea. Kwa masikitiko makubwa sana nathubutu kusema kwamba bado sijaona faida ya kibiashara ndani ya Muungano wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuelezea malalamiko yangu, naomba sasa nielezee juu ya Wabunge ambao wamebeba agenda ya kuibeza Zanzibar na Wazanzibari kwa ujumla. Kuna baadhi ya Wabunge humu wamebeba agenda ya kuibeza Zanzibar na Wazanzibari kwa ujumla na wamekwenda mbali mpaka kujiita kwamba wao ndiyo wababe wa Wazanzibari. Niwaambie tu, mbabe wa Wazanzibari ni Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein ambaye ndiye Rais wetu na hakuna mbabe zaidi ya huyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kueleza hayo, naomba sasa nijikite kwenye mchango wangu moja kwa moja na nitaanza kuelezea hali ya kiuchumi nchini. Ukurasa wa nane umeelezea viashiria vya kiuchumi vinaonesha kuwa katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Septemba, 2017, uchumi ulikua kwa asilimia 6.8. Sina mashaka na maelezo haya na kwa vile hotuba hii haijaonesha ni viashiria gani ambavyo vimepima ukuaji uchumi huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuangalie ripoti ya REPOA na takwimu ambazo imeonesha. Ripoti ya REPOA inaonesha kwamba mwaka 2014 asilimia 22 ya Watanzania walikuwa wanashinda na njaa wakati mwaka 2018 asilimia 27 ya Watanzania wanashinda au kulala na njaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ripoti hii pia imeonesha hali ya ajira nchini. Ripoti hii inaonesha kwamba vijana wa Kitanzania asilimia 43 walikuwa na imani kuwa Serikali itatengeneza ajira wakati mwaka 2018 ni vijana asilimia 31 tu ndiyo wenye imani kuwa Serikali itatengeneza ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ripoti hii pia inaonesha hali ya ufukara nchini. Kwa mwaka 2014 asilimia 64 ya Watanzania hawakuweza kumudu maisha yao wakati kwa mwaka 2018 ni asilimia 76 ya Watanzania hawakuweza kumudu maisha yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia tuangalie ripoti ya Serikali kupitia Taasisi ya NBS ambayo inaonesha hali ya udumavu kwa mwaka 2014 ni asilimia 34.4 ya watoto nchini walikuwa wamedumaa, wakati kwa mwaka 2018 asilimia 34.7 ya watoto nchini wamedumaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ripoti hiihii pia imeonesha vifo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)