Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi hii ya kuweza kuchangia katika hotuba ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kwanza kuchangia kuhusiana na suala zima la Tume ya Uchaguzi. Katika hotuba ya Waziri Mkuu alisema kwamba Tume ya Uchaguzi imekuwa ikifanya kazi kwa ufanisi, sasa ni ufanisi gani anaouongolea kama Tume hii mpaka sasa tumeiona ikiwa inatenda kazi kinyume na taratibu na kanuni zilizowekwa na sheria ambazo ziko wazi. Jambo la kushangaza zaidi Tume hii ipo chini ya Mwenyekiti ambaye ni Jaji, tulitegemea kwamba mtu kama Jaji angeweza kuisimamia hii Tume iweze kuwajibika na kufanya kazi zake wka kufuata taratibu na sheria na kanuni zilizopo.

KUHUSU UTRATIBU . . .

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuendelea na mchango wangu hapa kwenye suala la Tume ya Uchaguzi kuhusu taratibu ambazo zinatakiwa kufuatwa kila baada ya uchaguzi ni Daftari la Mpiga Kura linatakiwa kuboreshwa mara mbili baada ya uchaguzi kumalizika, mpaka sasa hivi tumeshuhudia kwamba Daftari la Mpiga Kura halijaboreshwa hata mara moja na sasa hivi ni mwaka wa tatu tangia tumalize uchaguzi uliopita. Sasa hii inatuwekea sintofahamu na tunaanza kuingia mashaka kwamba Tume wana mpango gani tunapoelekea kwenye uchaguzi wa mwaka 2020 kama mpaka dakika hii hakujafanyika taratibu za kuhuisha Daftari la Mpiga Kura .

Kwa hiyo, hiki ni kitu ambacho kimetuletea mashaka na tunaomba Serikali iliangalie hili waweze kulichukulia hatua haraka iwezekanavyo ili tunapoelekea kwenye uchaguzi hili zoezi liwe tayari limeshamalizika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala lingine ambalo liko katika uwezeshaji wa uchaguzi (Electoral Support Program) ambao ni mradi kwa ajili ya kuwezesha uchaguzi. Lakini kitu cha kusikitisha kabisa ni kwamba huu mradi haujapatiwa pesa hata kidogo. Katika bajeti ya mwaka 2017/ 2018 bajeti ambayo ilipitishwa ilikuwa ni shilingi bilioni 10 lakini hawakupewa hata senti tano na mwaka huu pia bajeti cha kushangaza bajeti imeenda kupunguzwa by 50% badala ya shilingi bilioni 10 wakati ule sasa hivi wanapewa shilingi bilioni tano, sasa inakuwaje tunakuwa na mradi kama huu halafu hamna pesa yoyote ambayo inaenda kupitishwa, ningeomba hili pia liangaliwe kwa sababu mradi wa uwezeshaji wa uchaguzi ni suala muhimu sana na utahitaji kuwa na funds za kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ningependa kuongelea suala la Commission of Mediation and Arbitration (Tume ya Usuluhishi na Uamuzi). Nimeona katika hii hotuba ya Waziri Mkuu amesema kwamba kumekuwa na ujenzi wa Mahakama na ukarabati wa Mahakama mbalimbali lakini hamna sehemu aliyoongelea kuhusiana na suala hili muhimu la Commission of Mediation and Arbitration, tungeomba hili suala Serikali ilichukulie umaanani na umuhimu kwa sababu mpaka sasa hivi imejitokeza changamoto nyinig sana kuhusiana na suala la Tume hii ya Mediation and Arbitration, kwanza hamna majengo ya kutosha, mpaka sasa hivi tunachokiona ni kwamba unakuta wanakuwa na chumba kimoja ambako ndiyo wanafanya hiyo mediation na zinavyokaa kesi mbili hadi tatu; kwa hiyo, kuna kuwa na muingiliano kunakuwa hamna privacy, huku wanafanya mediation na huku pia yaani kusema kweli tunahitaji sana kuwe kuna majengo ya kutosha. Pia kuwe kuna staffing maana iko understaffed.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachoshangaa ni kwa nini Serikali inashindwa kuleta watumishi au kuajiri watumishi kwa ajili ya hii Tume ukizingatia tuna wanafunzi wengi ambao wana graduate, ishindikane vipi hawa watu washindwe kuajiriwa. Ningeshauri hili suala lingechukuliwa kama suala ambalo ni muhimu sana ikiwa kama kitengo cha kutaka kuhakikisha kwamba tunaimarisha eneo letu la utoaji haki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ningependa kuongelea suala la strong institution for sustainable development, tunahitaji kuwa na taasisi imara kwa ajili ya maendeleo endelevu. Nasema hivi ni kwa sababu taasisi zetu zinahitaji kuwa na uwezo wa kujiendesha, uwezo wa kujisimamia katika maamuzi yake, lakini kitu ambacho kinaendelea sasa hivi unakuta kwamba mfano mdogo tu naweza kuutoa ni Jeshi la Polisi. Jeshi la Polisi sasa hivi kinachoendelea ni kwamba mtu anaweza akachukuliwa akawekwa mahabusu kwa muda wa siku 14 pasipo kupewa haki yake ya kufikishwa Mahakamani. Kinachobaki wanakuambia kwamba wanasubiri maelekezo kutoka juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunapokuwa na taasisi kama hizi, zinakosa kujisimamia na kuweza kujiendesha bila kutegemea maamuzi ya mtu huyu mmoja, naomba niwakumbushe kwamba Ujerumani kulikuwa kuna Adolf Hitler, alikuwa anaingilia mifumo ya utoaji haki. Aliingilia hadi Jeshi la Polisi na ilipelekea hadi kukawa na machafuko. Hatutaki kufikia huko, sasa tunaomba ifike wakati taasisi zetu zijengewe uimara, ziweze kujitegemea zenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala lingine la mabadiliko ya tabianchi. Mabadiliko ya tabianchi ndiyo hapo ambapo tunakuta kunaweza kukajitokeza majanga kama mafuriko, lakini sasa kitu cha kushangaza ni kwamba hamna pesa za ndani zinazotengwa kwa ajili ya kitu muhimu kama hikiā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha muda wa Mzungumzaji)