Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu lakini la pili nimpongeze sana Rais Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri ambayo anafanya. Vilevile nichukue nafasi hii kumshukuru Waziri Mkuu kwa kazi ambazo anazifanya, ni haki yake kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijielekeze katika mchango, kwa kuwa dakika zangu ni kidogo nigusie katika watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI. Niiombe Serikali yangu tukufu, watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI wanapata taabu sana katika kupata matibabu yao. Niombe sana kila Halmashauri iweze kutenga fedha kiasi cha asilimia mbili au asilimia tatu wapewe watu wanaoishi na maradhi ya UKIMWI ili waweze kuunda vikundi ili waweze kujiendesha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninalisema hili kwa kuwa kuna mifano ambayo imetoka, baadhi ya Halmashauri wamepewa nafasi hizi na wamepewa fedha hizi wameweza kujiendeleza kwa makini na wameweza kujiwekeza kupata mpaka kadi za matibabu wao wenyewe na mitaji yao imekuwa mikubwa. Nimuombe Mheshimiwa Waziri kama hawa watu watapewa fedha kutokana na Halmashauri zetu na kuwe kuna sheria maalum ambazo Halmashauri hizi zilazimike kuwapa pesa watu hawa ili waweze kufikia hatua tunayotaka. Tukiwapa fedha tutaondoa utegemezi mkubwa kwa watu wenye kuishi na maradhi ya UKIMWI kwa sababu wanaweza kujitegemea, lakini Serikali inahitaji lazima iweze kuwainua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niligusie sana hili suala la watu hawa wanaoishi na maradhi ya UKIMWI na wanaoishi na VVU, hata ukitoa fedha kwenye mfuko wa Waziri Mkuu wakipewa hawa watu basi wanaweza kujiendesha kwa hali kubwa sana na wana uwezo mkubwa sana. Nimuombe Dada yangu Jenista aliangalie kwa makini ili aweze kuziā€¦ Halmashauri zote ziweze kutoa fedha kwa watu wenye kuishi naVVU.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende katika jambo la pili, suala la miradi ya maji. Miradi ya maji ndani ya nchi yetu inakwenda vizuri na uendaji wake vizuri ni kutokana na fedha za Mfuko wa Maji ambayo si fedha za bajeti. Fedha za bajeti zinazokwenda bado ni kidogo sana na niiombe Serikali iweze kuewekeza pesa za maendeleo za bajeti katika Mfuko wa Maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna fedha zetu za Mfuko wa Maji ambazo ndizo tegemeo kubwa katika miradi yetu ya maji. Sasa tuiombe Serikali iweze kukubaliana na Waheshimiwa Wabunge ili kuongeza shilingi 50 iwe shilingi 100 ili wananchi wetu waweze kupata huduma ya maji kwa makini. Mimi nashangaa sijui ni kwanini Serikali inapata kigugumizi kuongeza hii shilingi 50 ili itimie shilingi 100 ili Wananchi wetu waweze kupata maji ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ilani ya Chama cha Mapinduzi ilielekeza kabisa maji ni muhimu, sasa tunashangaa kama Serikali haiwezi kukubaliana na sisi Wabunge ambao tumetumwa na wananchi tuje kwenu ili tuweze kuiambia Serikali kwa yale ambayo tunayoyataka, tunashangaa Serikali inapata kigugumizi wakati hao wananchi wenyewe ndiyo wanataka hii fedha iongezwe ili wananchi wapate maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee na suala lingine la kilimo; sera ya nchi yetu imejielekeza katika uchumi wa viwanda. Ni kweli ni sera nzuri ambayo inaleta matumaini makubwa, lakini ili uchumi wa viwanda uende vizuri lazima kuwe na kilimo bora. Sisi mpaka sasa nchi yetu tuna ardhi nzuri ya kilimo, lakini hatujakaa vizuri katika suala la kilimo. Kwa hiyo, tukikubaliana kuimarisha kilimo cha uhakika basi ninaamini hivi viwanda ambavyo tunavyovitaka vitakuwa vinafanyakazi kwa uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiangalia suala la mradi wa kilimo hasa upatikanaji wa pembejeo, Mheshimiwa Waziri na Bunge lako tukufu lilipitisha uhakika wa unuaji wa mbolea wa pamoja lakini mpaka hivi sasa ule uendeshaji, upatikanaji wa zile mbolea bado ni tabu haujakuwa sahihi na kwa sababu moja, kwa kuwa leo Mheshimiwa Waziri wa Kilimo yupo ananisikia nimshauri nia halisi ya kufanya ili aweze kufika hatua hawa wakulima wetu wasiweze kupata taabu. Mheshimiwa Waziri nikushauri jambo dogo tu, huu ununuaji wa mbolea ni mzuri, lakini uweze kununua mbolea kwa wakati wote usingoje msimu wa kilimo ndipo uanze kuagiza mbolea. Hii mbolea inatakiwa iwepo kila wakati humu madukani Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.