Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naitwa Maria Ndila Kangoye, ni Mbunge wa Viti Maalum kutokea Mkoa wa Mwanza nikiwakilisha vijana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kuanza kwa kumshukuru Mungu kwa kuniwezesha kusimama siku hii ya leo hapa nilipo. Pia nipende kuwashukuru wapigakura wangu ambao ni vijana wa UVCCM Mkoa wa Mwanza pamoja na wanawake wa UWT ngazi ya Taifa kwa kunipa dhamana ya kuwakilisha vijana ndani ya Bunge hili la Kumi na Moja. (Makofi)
Mhehimiwa Mwenyekiti, napenda pia kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri inayofanya. Nampongeza sana Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli pamoja na wasaidizi wake ambao ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Manaibu Waziri pamoja na watendaji wote wa Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nijielekeze katika kuchangia hoja iliyopo. Kwanza, nianze kwa kusema kwamba naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja kwani hotuba ya Mheshimiwa Waziri imesheheni mambo mazuri yenye kuleta matumaini katika Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kwamba Kilimo kimeajiri takriban asilimia 70 ya Watanzania na wengi wao wakiwa ni vijana. Hivyo basi, napenda kuungana na Wabunge wenzangu wanaotokana na Kanda ya Ziwa hasa wale walioongelea zao la pamba kwa kusema kwamba ni kweli zao la pamba limeanza kupunguza uthamani wake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima wa pamba wamekuwa wakikatishwa tamaa na changamoto nyingi zinazolikabili zao hili. Baadhi ya changamo hizi ni ukosefu wa masoko ya uhakika, lakini kumekuwa na ucheleweshwaji wa pembejeo hususan mbegu na kumekuwa pia na usambazaji wa mbegu ambazo hazioti. Hii imewakatisha tamaa sana wakulima wa pamba. (Makofi)
Mheshimwa Mwenyekiti, labda kwa kwa kutoa mfano, tatizo hili limewahi kutukumba hata kule Wilayani kwangu Magu, katika vijiji vingi vikiwemo kijiji cha Shishani, Kabila, Mwamanga, Ndagalu na vingine vingi. Kwa kuwa Serikali ina mpango wa kujikita katika viwanda napenda kuiomba Serikali ifufue viwanda vya nguo ili kuweza kupata soko la ndani kwa wakulima wa pamba. Naamini viwanda hivi vitaweza kutoa ajira kwa vijana, kama Rais wetu alivyoweza kuajiriwa katika Kiwanda cha Mwatex enzi za ujana wake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia kwamba kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa nchi yetu, napenda kuipongeza Serikali kwa kuanzisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo. Naamini sasa vijana wengi waliojiajiri katika sekta hii wataweza kupata mikopo ya bei nafuu na kuweza kupanua kilimo chao kulingana na teknolojia ya hivi sasa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto nyingine kubwa inayomkabili mkulima wa Kitanzania ni ile ya kutozwa kodi nyingi mpaka mazao yake yanapofika sokoni. Namshukuru Waziri Mkuu, wiki iliyopita amesimama hapa mbele yetu na kutuhakikishia kwamba kodi hizi zitapunguzwa, na mimi ninachoiomba Serikali ni kwamba ianze kutekeleza agizo hilo kwa uharaka ili wakulima waanze kunufaika mapema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tatizo lingine kubwa. Wakulima hawa wanapofika masokoni, wanakutana na madalali. Madalali hawa wamekuwa kama miungu watu ndani ya masoko haya. Wao ndio wapangaji wa bei na wamekuwa wakitengeneza mazingira ya kukabidhiwa mazao haya; wao ndio wanaouza, ndio wanaopokea pesa na mara nyingi wamekuwa wakiwatapeli wakulima. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuiomba Serikali kuweza kuanzisha chombo maalum ambacho kitakuwa chini ya Halmashauri za Wilaya ambacho kitawatambua hawa madalali na ikiwezekana na wao walipishwe kodi kwa sababu hata hiyo pesa wanayopata haina jasho. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanda ya Ziwa hususan Mkoa wa Mwanza ni maarufu kwa ufugaji, lakini kumekuwa na uhaba wa viwanda vya kusindika nyama, maziwa na kuchakata ngozi. Naiomba Serikali itoe kipaumbele kwa kuanzisha viwanda hivi ili kuweza kunufaisha jamii ya ufugaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ifike mahali tuachane na kusafirisha mifugo, ila tujikite katika usindikaji wa nyama, maziwa na usafirishaji wa ngozi ambazo tayari zimekuwa processed. Hili ni suala ambalo linawezekana na nina uhakika kwa Serikali hii inawezekana kabisa. Labda kwa kutoa tu mfano, kuna Ranchi ya Kongwa hapa ya NARCO, imekuwa ikisafirisha nyama kutoka kwenye ranchi yake kwenda sehemu mbalimbali, hata kwenye maduka ya kuuza nyama (butcheries)yaliyoko Dar es Salaam.
Sasa ikiwa suala kama hili tayari lilishaanzishwa tena na vyombo vya Serikali, je, inashindakana vipi kuweka mlologo mzuri ili nyama ya ng‟ombe inayotoka Mwanza iweze kufika Dar es Salaam ikiwa fresh na kuwafikia walengwa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuhitimisha mchango wangu kwa kuiomba Serikali kuiangalia Wilaya ya Ukerewe kwa jicho la pekee. Ukerewe ina visiwa 38; kati ya hivyo, 15 ndivyo vyenye makazi ya kudumu na 23 ni makambi ya wavuvi; na wavuvi wengi ni vijana. Nasikitika kusema kwamba vijana hawa ambao ni wavuvi wamekuwa wakihangaika kutafuta masoko mbali na Ukerewe, ukizingatia kwamba viwanda vya samaki vipo Musoma na Mwanza. Vilevile tukiangalia hali ya usafiri wanaotumia siyo usafiri wa uhakika, yaani usafiri ule siyo salama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mara nyingi tumekuwa tukiwaokota pembezoni mwa ziwa na hii kwa kweli…
MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.