Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini

Hon. Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami naomba niungane na Wabunge wote wazalendo wa nchi hii ya Tanzania ambao wanampongeza Rais wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme, kumekuwa na maneno mengi katika jambo hili. Tukitizama hoja ambayo ipo hapa ndani ya Bunge letu Tukufu, hoja yenyewe kimsingi inatutaka sisi Wabunge kwa pamoja tuungane na Watanzania wenzetu ambao kwa mara ya kwanza wameshuhudia uzalendo, ujasiri na hekima na busara iliyotumiwa na Rais wetu katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi na mwenendo mzima wa utendaji kazi wa Serikali katika kulinda rasilimali za Taifa letu la Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika historia ya nchi yetu ya Tanzania, nashukuru leo Mheshimiwa Tundu Lissu amezungumza vizuri sana, ameona kuna umuhimu tunapompongeza Rais Dkt. John Pombe Magufuli tuwapongeze na Marais waliotangulia pia. Ingawa jana Tundu Lissu huyo huyo aliwadhalilisha pia Marais waliotangulia katika hoja hii hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ninachojifunza hapa ni kwamba hata dhamira ya mioyo ya wenzetu kumbe wanakubaliana na kazi nzuri aliyoifanya Rais pamoja na watangulizi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa nini? Marais waliotangulia walianzisha hoja hii kwa namna moja ama nyingine kwa kuunda Kamati zile zinazojulikana, lakini kazi iliyokuja kuendelezwa ambayo pia tunaipongeza vizuri leo, ni kitendo cha Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli Rais wetu, kuziweka kwanza ripoti hizo zote mbili hadharani na zikasikika na Watanzania wote. Pili, ni kuanza kuchukua hatua kwa ripoti ile ya kwanza. Tatu, ni kutoa maagizo makubwa kwenye ripoti hii. Kwa hiyo, Watanzania wote… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)