Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini

Hon. Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru kwa kunipa dakika tatu za kuunga mkono Azimio la Bunge kwa ajili ya kumpongeza Rais kwa hatua madhubuti alizochukua kuhakikisha kwamba nchi yetu inanufaika kikamilifu na uchimbaji wa madini hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli viongozi wote waliotangulia, naomba unyamaze usiniite, nitakutakana halafu nitaonekana sina maana. Eeh kwa sababu wewe unaniita jina la nini mimi mume wako niache nichangie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli viongozi wote waliotangulia waliunda Tume na ni kweli wakati ule sheria zetu zilikuwa zina wa-favour sana wawekezaji kwa wakati ule wa 1977, 1979, tulihitaji wawekezaji waje wawekeze kwenye sekta ya madini ambapo hawakuwepo wawekezaji wakubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tume zile zilizoundwa zilifanya kazi zake lakini Tume ya Mheshimiwa Magufuli kwa nini tunaipongeza, imefanya kazi na yeye mwenyewe ameenda mbele zaidi. Ameweka wazi ripoti za hizi Tume tena hadharani na kila mtu amezisikia tofauti na Tume zilizoundwa hapo kabla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa hatua hii kubwa kwa sababu haiwezekani Taifa lisimpongeze kiongozi wake anapochukua hatua zinazoonekana kwa macho. Hapa nilisema na leo tumegawana, ukishindwa kupongeza, utapongeza wale wanaotuibia na imekuja hiyo wazi kabisa kwenye Bunge hili, umeona ripoti za Maprofesa, wataalam zinaitwa za upuuzi kwa sababu kuna watu wanaunga mkono upande mwingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sisi ambao tuko kwenye Bunge hili ambao tunaona kazi nzuri iliyofanywa na Rais, nataka niwaambie tu, siyo msemaji wake lakini nimeona kuna clip Mzee Lowassa naye kampongeza Rais. Sasa sijui hawa ambao wanakataa kumpongeza Rais wanaitoa wapi, kwa sababu hata Sumaye amempongeza Rais na ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA. Kwa hiyo, ndiyo maana tunasema Bunge zima lina wajibu wa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa hatua kubwa alizozichukua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kurekebisha sheria, hivi kwenye Bunge la Bajeti hili, umeletwa Muswada wa kurekebisha sheria ya madini? Labda uelewa wangu mdogo, kwa sababu haiwezekani ulete Muswada sasa hivi turekebishe hizo sheria wakati tuko kwenye Bunge la Bajeti. Hapa tunachukua hatua ya kumpongeza Mheshimiwa Rais halafu tuitake Serikali ilete haraka Miswada ya kurekebisha.