Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama kueleza hoja moja tu, baadhi ya watu mmezungumza juu ya utendaji kazi wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme kama ifuatavyo, ukijua kazi inayofanywa na Idara ya Usalama wa Taifa yale mliyoyazungumza humu ndani msingeyazungumza, ninayo sheria hapa ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1996 nataka nikusomeeni kwa mujibu iliyopitishwa na Bunge, nataka nikusomeeni kazi za Idara ya Usalama wa Taifa, ukizisikiliza hayo yote mliyoyasema hayahusiani na Idara, fulani kapotea police case, fulani kaumizwa police case, haihusiani na Idara ya Usalama wa Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kifupi kazi ya Idara ya Usalama nchi yoyote ni kutafuta habari na kuishauri Serikali.

Nasema imeandikwa kiingereza Mimi nitasema kwa Kiswahili kwa sababu ili Watanzania wanaosikia waliopo hapa wote tupate uelewa mmoja kifupi ninachotaka kusema hoja mlizozitoa kuhusu Idara hazihusiani na Idara, hoja mlizozitoa kuhusu Idara haishauri Serikali mambo ya uchumi, haifanyi nini, haifanyi nini hamna ushahidi, katika nchi zote duniani Idara ya Usalama inatafuta habari nakuishauri Serikali yake kimya kimya (Makofi).

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana hakuna nchi utasikia msemaji wa Idara ya Usalama wa Taifa kasema hili, kasema hili, hakuna kitu kama hicho, kwa hiyo unaposema Serikali hawakuishauri unao ushahidi?

Sasa Sheria inasema hivi; “Subject to the control of the Minister the functions of the service shall be” shughuli zimewekwa nne;

(a) to obtain, correlate, and evaluate intelligence relevant to security (kukusanya habari, kutafuta habari na kuzifanyia tathimini) wanapofanya hayo hawayafanyi kwenye mkutano wa hadhara.

(b) To cooperate as far as practicable and necessary with such other organs of state (kushirikiana na vyombo vingine vya Idara zinazoshughulikia na usalama wa nchi), mna ushahidi hawana ushirikiania nao.

La tatu, linasema; to advise Ministers, where the Director-General is satisfied that it is necessary to do so (kuwashauri Mawaziri, kuishauri Serikali).

La nne, inasema to inform the President, and any other person or authority which the Minister may so direct, of any new area of potential espionage, sabotage, terrorism or subversion. Haya yote haya mambo ya kuhujumu uchumi ya nini, nini yanafanywa kimya kimya hakuna nchi inaita mkutano wa hadhara na kusema jamani tumevamiwa, hakuna nchi inaita mkutano wa hadhara na kusema tumefanya hivi, tumefanya hivi ninaomba Waheshimiwa Wabunge...

Mdogo wangu Zitto nakuheshimu sana, nimepewa mimi nafasi ya kuongea, ulipewa nafasi ya kuongea, hivi kwa nini mna-disturb wenzenu wakisema.

Sasa kwa sababu ya dakika tano nataka nifunge pia kwa haya maneno yamo ndani ya sheria inasema hivi; “It shall not be a function of the service (haitakuwa shughuli ya Idara ya TISS) (a) to enforce measures for security; mambo ya mabavu mabavu kushika, kumkamata huyu haitakuwa kazi yake. (Makofi)

(b) Inasema; to institute..., sikilizeni nikupeni darasa.(Makofi)

(b) Inasema haitakuwa shughuli ya Idara to institute surveillance of any person or category of persons by reason only of his or their involvement in lawful protest, haitakuwa kazi ya Idara ya Usalama wa Taifa kumchunga chunga mtu, kumfuata fuata imo ndani ya sheria. (Makofi).

Kwa hiyo, kifupi ninachotaka kusema ndugu zangu, tukitaka kusema mambo mazuri yanafanywa na Idara hii mashahidi ninyi mimi nataka kutoa mfano, palikuwa na kilio mahala palikuwa kuna msiba, watu waliofiwa wamenuna, wakataka kumpiga kiongozi wa chama, wakamwambia wewe ndiye umesababisha mtu wetu afe, alitoroshwa na watu wa Idara ya Usalama nini hamjui? (Makofi/Kicheko)

Kwa hiyo, tatizo mkiambiwa yale mnayoyajua yanayowauma mnapiga kelele.

Mheshimiwa Naibu Spika, Nakushukuru.