Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hiyo na kwa ajili ya muda niende kwenye mambo makubwa tu yanayohitaji ufafanuzi, yale mengine yaliyo ya maoni niseme tu tumeshapokea maoni hayo tutayafanyia kazi kiutawala kwa ukubwa wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikianza na hoja hii ambayo ilikuja kama swali anayoisemea Mheshimiwa Msigwa kama Mheshimiwa Rais alichozindua ni e-passport ana ni e- immigration.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili lilirudiwa kukosewa hata siku ile Mwenyekiti wa Kamati husika aliposema na niliona Wabunge wakishangilia wakisema kwamba tungeanzia kuzindua e-immigration ndio tuzindue e-passport.

Mheshimiwa Naibu Spika, e-immigration ni set na hivi vingine tunavyoendelea navyo ni subset za e-immigration, so the whole system ni e-immigration ndani yake kuna e- passport, kuna e-visa, kuna e-permit, kuna e-gate kwa maana hiyo Mbunge, Mwenyekiti wa Kamati ile aliyosema anashangaa kwa nini tumezindua e-passport badala ya e- immigration ni confusion, is a total confusion kwa sababu e-immigration hamna sehemu utaenda kuishika kwamba hii ndio e-immigration. Lakini tunachosema…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri naomba utusaidie kwa sababu jambo hili limesha pelekwa kwenye Kamati ili nyaraka zipelekwe huko, mimi ningeomba ujielekeze kwenye mambo mengine kwa sababu hili tayari tutaletewa ufafanuzi na kamati mahsusi.

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, lakini kuna mambo ambayo yalikuwa ya Wizara kwa mfano anaposemea hii ilikuwa inauzwa pound nane hii ni dola 68. Dola 68 hii siyo arrangement ya supplier, hii ni bei ya immigration ambayo sisi kama waendesha mradi tuna amri ya kutoa passport bure kama tunavyotoa kitambulisho cha Taifa ama kuuza, kwa hiyo tumepiga hesabu tukaona hii tunatakiwa tuuze ili kuweza kutengeneza maduhuli lakini pia na ku-cover gharama za mradi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa umetolea maelekezo na mimi wakati wa kusimama nilikuwa natamani nimwambie Mheshimiwa Msigwa aweke hizo nyaraka leo leo lakini mmempa muda mrefu zaidi basi ngoja aende kwenye hiyo ya muda mrefu zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukienda kwenye hili la ulinzi wa Waheshimiwa Wabunge, hoja ya viongozi kupewa ulinzi ni hoja ya msingi na sisi kama Serikali hatuwezi tukapingana na hoja ya ulinzi kwa viongozi na hoja ya ulinzi kwa wananchi ni hoja ya msingi ambayo sisi kama viongozi hatuwezi tukapinga hoja ya ulinzi kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Lakini jambo moja tu ambalo naomba nitoe rai kwa Waheshimiwa Wabunge ni kwamba kuna miundombinu ambayo lazima iwe imefanyika katika nchi ili uweze kufanya ulinzi wa Mbunge mmoja mmoja. Kwa mfano kwa hapa Dodoma sisi tayari tulisha kubaliana na Kamati na tulikubaliana na tulitoa taarifa kwamba maeneo wanapokaa Wabunge tutaimarisha doria punde Wabunge wako hapa, na maeneo ambako kuna Wabunge wengi wanakaa kwa pamoja tutaweza kutengeneza utaratibu wa askari ambao watakuwa katika maeneo hayo ama kwa njia ya doria ama kwa kuwaweka katika station hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini utaratibu wa kuwa na ulinzi kwa Mbunge mathalani kwa kila jimbo ni jambo ambalo linahitaji miundombinu kwanza kabla hujaweka utaratibu huo. Lakini hata hapa kuna maeneo mengine ambako Wabunge wanakaa. Kwa taratibu za kiusalama lazima utengeneze miundombinu kwanza kwa sababu si kila eneo unaweza ukam–station askari, unaweza ukamuweka kwenye risk ya kushambuliwa hasa katika maeneo ambayo watu wangeweza kutaka hata kuchukua silaha hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maana hiyo wazo kama hilo kufika Serikalini ni jambo jema, ni wazo ambalo ni la kitaifa na sisi tungeomba Wabunge waelewe kwamba jambo hilo linahitaji miundombinu kwanza kabla hujaweza kupeleka ulinzi katika eneo hilo. Kwa mfano nchi zingine ambako wanafanya ulinzi wa aina hiyo, Mbunge akishachaguliwa kuwa Mbunge hakai eneo alikokuwa anakaa, anakaa wilayani kama mkuu wa wilaya anavyokaa na kwa namna hiyo unaweza ukasema hili ni eneo la viongozi unaweza kupeleka ulinzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwetu sisi katika nchi yetu utaratibu huo haupo na hata sheria yake haipo kwa maana hiyo kama jambo hilo litakubalika kama Taifa kuna miundombinu mingi sana ambayo inatakiwa ifanyike na hiyo ndiyo ingeweza kuwa njia njema ya kulifanyia jambo.

Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nizitakie kila la heri timu zinazocheza weekend hii hasa Simba kwasababu mara ya mwisho Simba kushiriki mashindano haya Zitto Kabwe alikuwa bado yuko CHADEMA.