Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, napongeza na naunga mkono taarifa ya Kamati. Ningependa kuongelea juu ya msongamano wa wafungwa na mahabusu magerezani yamefikia mahali pa kuvunja haki za binadamu kwani inafikia mahali wafungwa na mahabusu kushonana kama vijiti vya kiberiti, kitu ambacho hukupelekea wafungwa kukosa haki ya msingi ya kulala na pia kuambukizana magonjwa. Msongamano huu pia umesababisha Serikali kutumia fedha nyingi kuwahudumia. Ningeshauri ugeuzwe kuwa nguvu kazi ya uzalishaji hivyo kuzalisha vyakula au huduma itakayoongeza pato la Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nishauri Serikali inapopeleka mabalozi nje iangalie uwakilishi bora wenye tija wa kutangaza na kutafuta fursa za kiuchumi, kwani Mabalozi ndio wanaotarajiwa kuiuza nchi yetu kimataifa. Nishauri Serikali kufanya upimaji wa kazi zilizofanywa na balozi ili kutathimini iwapo kuna haja ya balozi huyo kuwepo huko kwenye uwakilishi wa Serikali katika nchi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, niishauri Serikali kuangalia pya juu ya watoto wanaozaliwa magerezani, wasiishi maisha ya ufungwa ya mzazi. Serikali itafute njia ya kuwalea watoto hao na kuwapa haki za msingi za watoto ili wasijione nao kama wafungwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, niishauri Serikali kuwajali wafungwa wenye ulemavu na wenye maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa kuwapa lishe bora pia kuwakinga na magonjwa nyemelezi.

Mheshimiwa Naibu Spika, niishauri Serikali kuangalia upya mpango wa ulinzi wa Wabunge ambao wamekuwa wakikamatwa kwenye maeneo ya Bunge kinyume na kanuni za Bunge, hivyo suala hili limekuwa kero sana kwa Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, niishauri Serikali kuwahisha fedha zinazoidhinishwa na Bunge kwa wakati, nashauri Serikali itambue uhitaji wa Wizara hii kwani ni nyeti sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, niishauri Serikali kuboresha nyumba za askari magereza kwani zina hali mbaya sana, zinapunguza morali ya kazi kwa askari hao.