Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia kuhusu Maafisa kupelekwa Ubalozini. Napendekeza kuwa kwa kuanzia Serikali ingepeleka Maafisa maeneo ya kimkakati hasa nchi za South-East Asia kama Korea, China na pia nchi au vituo ambavyo ni multiple kama Sweden au Ujerumani ambako Ubalozi unafanya kazi nchi zaidi ya tano.

Mheshimiwa Naibu Spika, naendelea kupendekeza umuhimu wa kufungua ubalozi mdogo kwa kuanzia Lubumbashi na Guangzhou. Jambo hili ni muhimu hasa ukizingatia biashara iliyopo katika ya nchi yetu na maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.