Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuchangia.

Kwanza kabisa nitoe pongezi kwa vyombo vya ulinzi na usalama kwa kazi nzuri wanayoifanya kwa kutunza amani. Pili, nashukuru sana na natoa pongezi kwa viongozi wote waliotangulia na waliopo kwa kutunza amani ya nchi yetu kwa sababu nchi ya Tanzania licha ya matatizo mbalimbali yaliyopo lakini bado ina amani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine naomba sana tena sana na nashukuru tuwe na amani na utulivu humu Bungeni mara tunapochangia hoja zetu Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo naomba kuchangia ni Wabunge wote tuweze wakati wowote tunapochangia tuweze kufuata Kanuni, Sheria na Taratibu za Bunge. Tukiweza kufuata Kanuni, Sheria na Taratibu za Bunge halitajitokeza tatizo lolote humu Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine lililoongelewa kwenye Kamati nasi wenyewe tunaliongelea hasa Wabunge wote naamini wataafiki ni Wabunge wote kupewa semina kuhusu mambo ya Kanuni, kwa sababu Wabunge wote wakipewa semina kuhusu mambo ya Kanuni Kiti kitakachokuwa kimekaa hapo ulipokaa naamini hakitasumbuliwa kwa sababu wote wataheshimu Kanuni na Taratibu za Bunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo lilikuwa linasumbua ni Shahidi kuitwa alafu Shahidi haonekani. Ili utunze amani na utulivu na haki ya binadamu unapoitwa kwenye Kamati ya Maadili ni vizuri uheshimu, ufike kwa wakati muafaka ambao unapangiwa, kuliko kuanza kutumiwa Polisi kukamatwa siyo vizuri. Kwa hiyo, naomba kuwa licha ya Wabunge kupewa Semina naamini kuwa tutafuata Kanuni na Taratibu za Bunge kuweza kufika kwa wakati muafaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa jinsi unavyoendesha Bunge wewe mwenyewe na Wabunge tukifata, narudia tena tukifata Kanuni na Sheria na Taratibu za Bunge na upendo ukitawala humu Bungeni tutakuwa na amani na utulivu mkubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongee hayo, ila kwa kumalizia nirudie kuwashukuru na kuwapa pongezi vyombo vya ulinzi kwani hivi karibuni lilikuwepo wimbi la watoto kupotea kwenye mazingira ya kutatanisha, ila nashukuru sasa hivi naona wimbi hili la watoto kupotea limepungua. Kwa hiyo, hii inadhihirisha kuwa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vinafanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo machache naunga mkono hoja, namalizia kwa kusema kuwa naomba tufuate Kanuni, Taratibu na Sheria za Bunge tutaendesha vizuri Bunge letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.