Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikushukuru wewe lakini pia nimpongeze Mzee wangu Mheshimiwa George Huruma Mkuchika kwa kupewa dhamana hii ya kuongoza Wizara ya Utumishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na suala la Wizara hii ya Ulinzi, kwangu kule Tandahimba kuna mambo yanafanywa na Askari wa Jeshi la Polisi, mambo ya hovyo kabisa. Mfano mdogo miezi mitatu iliyopita Askari Polisi wa Usalama Barabarani wamekuwa wakiwakamata vijana na kuwapiga. Sasa sijajua PGO ndiyo inataka hivyo au namna gani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hili jambo mara kadhaa nimewahi kumwambia Waziri mwenye dhamana kwamba DTO wa Tandahimba mambo anayofanya Tandahimba hayako sahihi. Sasa sijui kama kuna sheria inamwongoza Askari Polisi anapokamata mtuhumiwa ampige. Hili limekuwa ni jambo ambalo linalojirudia kwa Jimboni kwangu, mara kadhaa anawachomekea magari vijana wa bodaboda. Hii ni hali ya hatari sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri wakati atakapokuja atatuambia kwamba maelekezo aliyoyatoa sasa yamekaa namna hii au namna gani. Hata hivyo, ukienda Dar es Salaam pale sijajua au operation au ni kitu gani, ukiingia Mtaani Askari ambao hawana uniform wanakamata dereva bodaboda, ananyang’anya funguo kabla ya kumwambia jambo lolote lile, wakati mwingine hawajulikani kama hawa ni Askari au lah! Sasa ni vema kwa sababu mna bodaboda ambazo Askari wake wanavaa uniform wale wanafahamika vizuri mnaporuhusu Askari wanakwenda mtaani hawana uniform, wanakamata hovyo, mnahatarisha hata usalama wa raia wale wanaoishi mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, limezungumzwa hapa wakati wanazungumza suala la ulinzi wa Wabunge, jambo lililotokea kwa Mheshimiwa Lissu ni jambo la fedheha kubwa sana kwa Taifa letu. Ni jambo ambalo kwa namna moja au nyingine sijui kama Wabunge tunaona uzito wake. Limezungumzwa sana kwenye Bunge hili, lakini bado Wizara mpaka leo waliofanya matukio yale hakuna maelezo yanayojitosheleza kwamba wale watu wakoje.

Mheshimiwa Naibu Spika, maelezo ambayo yako clear kabisa, eneo la tukio ambalo Mheshimiwa Lissu amepigwa risasi ni eneo ambalo wanakaa Mawaziri, Mheshimiwa Naibu Spika unaishi pale, lakini vyombo vya ulinzi vinakuwepo pale, lakini mpaka leo jambo hili la Mheshimiwa Lissu limekuwa kizungumkuti halizungumzwi kwa mapana na kuonekana ufumbuzi wake unakuwaje. Leo kama Mheshimiwa Waziri jambo la Mheshimiwa Lissu analiona ni la masihara hili leo linatokea kwa Wapinzani kesho inawekana Wapinzani tukachukua nchi. Je, likitokea kwenu tuliangalie kama tunavyoliona hili? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati nimeona imeshauri jambo jema sana na nione sasa kuwe na umuhimu kama wenzetu wa Kenya, Wabunge wanalindwa mpaka majumbani kwao kuna ulinzi wa Jeshi la polisi kwa nini Tanzania tusiige majirani zetu pale. Kamati imeshauri vizuri imezunguza kwa uhalisia kwamba Wabunge wakati mwingine tunapotekeleza majukumu yetu tunapotetea rasilimali za nchi, wapo watu wanaoiba hawawezi kutuacha salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni vema tuone kwamba Bunge hili linaona na Wizara zione kabisa kwamba kuna umuhimu wa Wabunge kuwa na ulinzi wanapokuwa Majimboni lakini ikiwezekana hata tunapokuwa Dodoma hapa. Haya matukio mengine yanayotokea kama tunakuwa na ulinzi wa Jeshi la Polisi yawezekana kabisa yasitokee. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo jingine zipo Balozi zetu ukienda China kule kuna Maafisa wa Ubalozi hawapo, lakini bado hakuna hawajawapeleka watu wa kwenda kuziba nafasi zile. Sasa sijui kwenye Diplomasia ya uchumi kwenye jambo hili likoje, Waziri wa Mambo ya nje nadhani anaweza kutusaidia na hii siyo China tu, zipo nchi hata ukienda South Africa, mambo haya yako hivyo.