Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa niipongeze taarifa ya Kamati na kuunga hoja mkono kwa kazi nzuri iliyofanywa. Pili, niipongeze Serikali ya Awamu ya Tano ya Chama cha Mapinduzi chini ya uongozi mahiri wa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kupambana na kuziba mianya yote ya upotevu wa fedha na hatimaye kuboresha huduma za afya na elimu nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli usiopingika kwa MSD inafanya kazi nzuri sana ya usambazaji wa madawa katika hospitali mbalimbali nchini kwa wakati. Niombe Serikali yangu sikivu iweze kuongeza fedha katika bajeti ili taasisi hii iweze kutekeleza majukumu yake vilivyo. Naomba niipongeze tena Serikali kwa kazi nzuri iliyofanya ya kuhakikisha inapiga vita uingizwaji wa dawa za kulevya nchini. Hali hiyo imesaidia sana nguvu kazi ya Taifa isiendelee kupotea na pia kwa mkakati mzuri wa uanzishwaji wa sober houses ili kuwasaidia vijana wote walioathirika na matumizi ya madawa haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kuwa mtoto wa kike hasa wa kijijini wanakosa siku tano mpaka saba kuhudhuria shule pindi anapokuwa kwenye siku zake. Ndiyo maana mimi na Wabunge wanawake wote waweze kupaza sauti ili pale Serikali yetu itakapopata uwezo uweze kutazama jambo hili kwa jicho la tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu sasa Wizara ya Elimu imekuwa Wizara ya matamko na nyaraka hali inayopelekea kushuka kwa elimu. Takwimu zinaonesha mpaka sasa ufaulu unazidi kushuka hasa katika elimu ya sekondari. Ni asilimia 28 tu ndiyo wanaopata daraja la kwanza hadi la tatu na asilimia 72 wanapata daraja la nne na sifuri. Iko haja ya kutazama mifumo ya utolewaji elimu ndani ya Wizara hii kwani bila hivyo tutakuwa tikizalisha nguvu kazi duni na hafifu.