Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, vituo vya afya vingi vilivyojengwa kwa nguvu za wananchi Mkoani Ruvuma vingi vimefikia renta, havijaisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali itenge fedha kwa ajili ya kumalizia hivyo vituo vya afya ili kuokoa nguvu za wananchi zilizotumika, lakini pia kuboresha huduma ya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na Sera ya Taifa ya Elimu Bure kumekuwa na changamoto ya upungufu wa madarasa. Ninashauri Serikali yangu kuweka mkakati madhubuti ambao utalenga kuongeza madarasa katika shule zote zenye upungufu wa madarasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa walimu mashuleni umekuwa ni kero kubwa sana. Shule nyingi hazina walimu wa kutosha. Kutokuwa na walimu wa kutosha ni sawa na kuandaa chakula kizuri ambacho hakina chumvi. Athari ambayo itajitokeza katika Taifa hili baada ya miaka mitano ni kuwa na kizazi ambacho hakitakuwa na elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu afya, hospitali ya Wilaya ya Mbinga ina upungufu mkubwa wa wodi kwa ajili ya akina mama wanaosubiri kujifungua na wale ambao wameshajifungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi, naomba Waziri wa Afya aje katika Hospitali ya Mbinga, Mkoani Ruvuma ajionee mwenyewe adha ambayo wanaipata wanawake hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kuongeza bajeti katika sekta ya afya hususani madawa na vifaa tiba, lakini bado madawa hayatoshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sanaa, nampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupiga marufuku kwa wasanii wanawake kuvaa nguo ambazo ni kinyume na maadili yetu sisi Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naomba hoja na maoni yangu mbalimbali yaingie kwenye Hansard.