Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata fursa hii ya kuchangia mfano wa utoaji wa huduma ya afya nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na suala la ukatili kwa watoto; kumekuwa na changamoto kubwa ya ukatili dhidi ya watoto hasa wa chini ya miaka mitano. Inapotokea mtoto huyu anapata jaribio la kutendewa ukatili au jaribio la kubakwa na anapotakiwa kutoa ushahidi Polisi inaonekana kuwa ushahidi hautoshelezi na hivyo watuhumiwa wengi kuachiwa huru, hali hii inaongeza sana matukio ya ubakaji

Mheshimiwa Mwenyekiti, huduma kwa wajawazito; pamoja na Serikali kuonesha msisitizo wa huduma ya bure kwa wajawazito bado kumekuwa na changamoto kubwa ya vifaa vya kujifungulia hasa katika maeneo mengi ya vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zahanati zetu zimechoka sana na maeneo mengine hata maji hakuna hii ni hatari sana wakati mama anakwenda kujifungua. Pia vitanda vya kujifungulia ni changamoto kubwa kwenye zahanati zetu, vingi vimechakaa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile nizungumze suala la msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali za Mikoa na Wilaya; hili limekuwa tatizo kubwa kwa kuwa zahanati zetu hazijaboreshwa vya kutosha, hivyo wagonjwa wengi kukimbilia hospitali za mikoa na kusababisha msongamano mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la upungufu wa Madaktari Bingwa bado ni tatizo kubwa hasa kwa upande wa akinamama na watoto. Naomba Waziri anapokuja kuhitimisha aniambie na hizi ajira mpya 2018/2019 wamejipangaje kuongeza idadi ya Madaktari katika hospitali zetu ili kusaidia tatizo hili la msongamano wa wagonjwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tatizo la MRI- Scan kwenye hospitali zetu na hiyo kusababisha vifo visivyo na sababu kwa magonjwa yasiyoweza kugunduliwa kwa vipimo vya kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lishe; kumekuwa na tatizo kubwa la lishe, hivyo kuendelea kupata magonjwa kama kisukari, shinikizo la damu, ongezeko la uzito kwa watoto wadogo na watu wazima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Waziri anapokuja kuhitimisha aniambie kama Wizara wana mkakati gani wa kutoa elimu ya afya ili kuokoa Taifa letu.