Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la elimu; kwa sasa elimu yetu nchini imekuwa ni bure kuanzia ngazi ya msingi na sekondari. Suala hili limekuwa na mkanganyiko mkubwa kwani mapokeo ya wananchi wanajua kwa sasa hakuna mchango wowote ambao wanatakiwa kulipa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la Walimu kupandishwa, ni utaratibu tuliozoea katika nchi yetu Mwalimu anapojiendeleza anategemea kupandishwa daraja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la vyuo, kuna baadhi ya mikoa haina chuo hata kimoja katika kozi mbalimbali kitu ambacho kinakuwa ni changamoto kubwa kwa wanafunzi wanaohitimu katika maeneo mbalimbali. Ushauri wangu kwa Serikali kuhakikisha vyuo vinajengwa kwenye mikoa mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, madai ya Walimu, jambo hili limekuwa changamoto sana kwa Walimu wetu. Jambo hili ni hatari kwani sote tunatambua ualimu ni karama hivyo kutapelekea matokeo mabaya katika shule zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kukariri madarasa, jambo hili ni vizuri Serikali ikafanya tafiti za kutosha kabla haijazuia kwani suala hili lina athari kubwa sana kwa watoto wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa Wauguzi; baada ya Serikali kuja na suala la vyeti feki kumebaki na upungufu mkubwa wa nafasi mbalimbali katika hospitali nyingi nchini kwani jambo hili ni hatari sana kwa kitengo hiki muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la uzazi wa mpango; suala hili limekuwa na changamoto kwani elimu kwa watu wa vijijini bado haijatolewa kikamilifu, lakini pia Serikali ifanye tafiti juu ya baadhi ya njia za uzazi kwani zinalalamikiwa sana kuwa zinaleta madhara.