Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, niunge mkono taarifa ya UKIMWI na nipongeze uwasilishaji mzuri. Nipende kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali kuiwezesha Mamlaka ya Udhibiti wa Madawa ya Kulevya kupata vitendea kazi vya kisasa ili kuweza kuenda sambamba na vitendea kazi vinavyotumiwa na wahalifu. Serikali iwe sober house zake za binafsi ni ghali mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri Serikali kuipa meno Mamlaka ya Kudhibiti UKIMWI, kuwapa nguvu na mamlaka ya kufanya kulingana na uwezo wao. Serikali iwaongezee rasilimali watu ili kuwezesha utekelezaji wa kazi au majukumu yao kwa urahisi na kwa ufanisi. Nipende kuishauri Serikali kutoa waraka maalum ili kuwezesha halmashauri zote kuunganisha shughuli za UKIMWI kuunganishwa na madawa ya kulevya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, UKIMWI una vyanzo vingi vya kupata hasahasa wanaojidunga wamekuwa chanzo kikuu na hivyo suala hili linatakiwa kuangaliwa kwa makini ili kutoa elimu kwa vijana wetu jinsi ya kuishi maisha ambayo yatawaweka mbali na magonjwa hayo ambayo yana punguza nguvu kazi ya Taifa. Nishauri Serikali kuongeza bajeti ya UKIMWI na madawa ya kulevya. Niiombe Serikali kuwezesha waathirika wa UKIMWI kupata lishe kwani waathirika wanashindwa kupata lishe ili waweze kumeza dawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali kuweka mpango maalum wa utoaji dawa za magonjwa nyemelezi yanayotibiwa na septrin na dawa hii haijaambatanishwa kwenye dawa za kufubaza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo dume ni sababu mojawapo kwani mwanamke hana mamlaka juu ya mwili wao na pia wanawake wengi waume wao wengi hutumia dawa za UKIMWI kwa siri na huzihifadhi ofisini. Niishauri Serikali kuanzisha au kuendeleza taaluma, mitaala ya kujifunza jinsi gani UKIMWI unavyoenezwa na pia kupunguza uwepo wa night clubs kwenye makazi ya watu.