Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Serikali kujikita kwenye pambano la kuufuta ugonjwa huu wa UKIMWI ifikapo mwaka 2030. Tunashauri kwa sasa tumekwisha toa elimu ya kutosha, ni vyema tujikite kuwahudumia waathirika kwa ukamilifu zaidi. Serikali kuongeza bajeti kwa fedha zetu bila kusubiri fedha za wafadhili, hatathamini ifanyike kila mwaka kwa kila mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ni vyema ikafanye maamuzi magumu kwa kutoa ajira ya kukidhi mahitaji kwenye upungufu wa watumishi vitendea kazi, rasilimali fedha, angalau kwa asilimia 75 ndani ya huduma ya afya, elimu – VETA, msingi na sekondari. Kwani hatua hii ngumu inawezekana ndani ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili gonjwa limekuwa na NGO’s nyingi wakichukuliwa kuwa ni eneo la kupatia mapato, hivyo uwepo uchunguzi na kuweka vigezo vya kusababisha upunguzaji wa hizi NGOs kuelekea mwaka 2030.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pawepo na utaratibu wa kuwadhibiti watu au familia zinazowanyanyapaa wenzao miongoni mwao, wanaobainika kuwa waathirika wa UKIMWI au madawa ya kulevya. Kutungwe Kanuni maalum ya kuwaweka hatiani na kupatiwa adhabu ya kutowajibika ipasavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wapo ambao wanasambaza gonjwa hili na kufikia kuwasababishia vifo, nao kuendelea kutamba. Wahusika hawa wanaumiza moyo kwa baadhi ya wananchi na kuchukua sheria mkononi. Ni bora Serikali ikaona namna ya kuwawajibisha watu hawa na walio ndani ya jamii yetu. Suala hili ni siri kubwa inahitajika katika kutolewa kwake taarifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.