Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya UKIMWI imepitwa na wakati, sera hii ya UKIMWI imepitwa na wakati kwani sera ya mwaka 2001 naishauri Serikali ihuishe sera hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya masuala ya UKIMWI ni ndogo nasikitika kuona Serikali inatenga fedha kidogo wakati ugonjwa huu ni janga la kitaifa. Hii inaonyesha kuwa Serikali haina mpango na kuona ugonjwa huu unatokomezwa. Naishauri Serikali kuhakikisha inatenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya kupambana na ugonjwa huu mbaya. Pia fedha zikitengwa zipelekwe kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya madawa ya kulevya; naishauri Serikali itenge pesa kwa ajili ya kujenga sober house ili kuwanusuru vijana wetu ambao wanashindwa kwenda kwenye private sober houses ambako wanatoza shilingi laki 400,000 kwa mwezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo dume unachangia sana katika ongezeko la ugonjwa wa UKIMWI. Hii inatokana na akinamama kutokuwa na uhuru na miili yao. Mfano, baba mlevi anatumia nguvu au analazimisha mama kufanya tendo la ndoa. Naomba Serikali iendelee kutoa elimu kwa jamii kupitia vyombo vya habari, lakini pia kupitia taasisi mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iandae program maalum mashuleni kuanzia shule za misingi, sekondari ya vyuo zinazohusika na masuala ya UKIMWI. Fedha zinazopelekwa kwenye mkoa kwa ajili ya semina au mafunzo halmashauri moja ili zitumike kwa ajili ya kununua dawa za magonjwa nyemelezi na virutubisho.