Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa nianze kwa kusema jambo moja, hatuwezi kufanya mapinduzi ya viwanda kabla hatujafanya mapinduzi ya nguvukazi iliyo bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo mambo mengi sana ambayo ni muhimu kwenye mapinduzi ya viwanda. Ukiachana na habari ya umeme na raw materials, lakini jambo lingine ambalo ni la msingi na ni nguzo kwenye mapinduzi ya viwanda ni pamoja na nguvukazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipata fursa ya kumsikia Mama Christina Lagade ambaye ni Mkurugenzi wa Shirika la Fedha la Kimataifa la IMF alipokuwa Ethiopia mwaka 2017 mwishoni, anasema nchi kama Tanzania, Kenya, Nigeria na Ethiopia yenyewe, pamoja na fursa zilizonazo za kupelekea uchumi wa viwanda, haziwezi kufikia huko kama hawatawekeza kwenye nguvukazi (competitive labour force).

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kuwa na nguvukazi kama mfumo wa elimu hau-reflect dira ya Taifa. Hivyo vitu vitatu vinategemeana; nguvukazi, mfumo wa elimu na dira ya Taifa ni vitu ambavyo vinategemeana kweli kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu awamu ya pili ianze mpaka sasa hivi, kiwango cha elimu yetu kinashuka kwa speed iliyopindukia. Sizungumzii idadi ya wanafunzi mashuleni, nazungumzia kiwango cha ubora wa elimu inayotolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepitia ripoti ya Shirika moja la viwanda la Kimataifa la UNIDO ambalo linaonesha kwamba asilimia 80 ya labor force katika Taifa letu ni unskilled. Mheshimiwa Waziri wa Elimu haya mambo unapaswa kuja na majibu, kwa sababu hatuwezi ku-invest, hatuwezi kuandaa kizazi kupeleka watu shuleni wakasoma halafu wakawa unskilled.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ATE (Association of Tanzania Employers), Shirikisho la Waajiri na wenyewe wamekuja na taarifa yao, wanasema 30% to 40% ya ajira wanazozitangaza watu wanakosa vigezo/sifa. Tafsiri yake hapa kuna mismatch, mismatch kwa namna gani, kwa maana ya kwamba watu tunaowazalisha wanapishana na mahitaji ya soko la ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vyema suala hili likaangaliwa kwa umakini mkubwa kwa sababu tunaweza tukawa tunahubiri kwamba ajira hakuna na wakati sababu kubwa inaweza ikawa ni tunapishana na mazingira ya sasa na uhitaji wa elimu tunaotakiwa kuupata kutokana na ushindani uliopo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kusikitisha zaidi ni kwamba elimu hii inashuka kwa kasi kipindi ambacho tunaihitaji kutokana na ushindani ambao tunao. Wakati huo huo, nchi zote ambazo zimefanikiwa katika mapinduzi ya viwanda zime-invest sana kwenye nguvu kazi. Zime-invest kwenye nguvu kazi kwa namna gani? Zime-invest kupitia elimu ya kati. Tunachemka kweli kweli, tumeshindwa kutengeneza uwiano sahihi wa nguvu kazi kupitia elimu ya kati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi ambazo zimefanikiwa kwenye mapinduzi ya viwanda kupitia nguvu kazi ya elimu ya kati wanafanya hivi; uwiano wa elimu ya kati na elimu ya juu ni moja ya ishirini mpaka moja ya hamsini kwa maana ya kwamba, kama kwa elimu ya juu kuna mtu mmoja basi elimu ya kati kuna watu ishirini au kama elimu ya juu kuna mtu mmoja basi elimu ya kati kuna watu hamsini lakini sisi ni vice versa. Kama elimu ya juu kuna watu watatu eti nguvu kazi kuna mtu mmoja ambaye ni elimu ya kati. Tume-invest sana kutengeneza managers tunaacha kutengeneza watendaji ambao ni watu wa elimu ya kati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka haraka, nimepitia kitabu cha Ally Mafuruki ambacho amekizindua mwaka jana Mheshimiwa Rais mwenyewe, ningeomba au ningependekeza kama Mheshimiwa Rais alikipeleka akakiweka kwenye draw, akifungue akisome kina majibu mengi sana ya matatizo yetu.