Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naishukuru Kamati yangu ya Guantanamo ambayo imeshiriki kwa namna moja katika kuleta taarifa hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mwanakamati nitajikita zaidi katika suala la elimu. Ni wazi kuwa Serikali yetu ipo katika hatua za kuelekea katika Tanzania ya viwanda, lakini hatuwezi kufikia Tanzania ya viwanda bila kuwa na wataalam ambao wataenda kuvihudumia hivi viwanda. Wataalam hao ni wanafunzi na hawa wanafunzi hawawezi kupata yale yanayohitajiwa kama hawatakuwa na walimu wazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi walimu wamekuwa na changamoto nyingi sana zinazosababisha mpaka morale ya kufanya kazi ipotee. Sababu mojawapo kwanza ni kudhalilishwa kwa walimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi walimu wanadhalilishwa sana kana kwamba hawana taaluma, leo hii na siku za nyuma baadhi ya ma-DC, ma-RC hata Wakurugenzi wamekuwa ni watu wa kuwadhalilisha walimu, wanawatandika fimbo, kuna walimu wameshadekishwa vyumba vya madarasa, kwa kweli hali hii inasababisha mpaka morale ya kazi ipungue. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala lingine la kushusha vyeo walimu. Hili suala limekuwa sasa hivi ni too much. Mwalimu mwenye professional yake, leo kwa sababu ambazo ziko nje ya uwezo wake, anashushwa cheo na Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya, eti tu kwa sababu shule imefelisha, je, anayefanya mtihani ni Mwalimu au mwanafunzi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba majibu ya Serikali, kazi au majukumu ya kushusha vyeo au kutoa nidhamu na maadili kwa walimu yako chini ya Tume ya Utumishi wa Walimu, sasa nataka nijue, hili jukumu la kushusha vyeo walimu linachukuliwa na Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya, je, mmeinyang’anya madaraka Tume ya Utumishi wa Walimu na kuwapa hawa viongozi wa Serikali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine linalochangia hadi kuzorota kwa elimu yetu ni kuchanganywa kwa kauli mbalimbali zinazotolewa na viongozi wetu wa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa juzi kulikuwa kuna kauli mbalimbali zinazotolewa na viongozi wa Serikali, mfano Mheshimiwa Rais alisema kwamba walimu wasihamishwe kutoka kituo kimoja kwenda kituo kingine mpaka pale atakapopewa mafao yake ya uhamisho. Ghafla kuna kauli imetolewa tena na Wizara ikisema kwamba kuna Walimu wanahamishwa kutoka sekondari kwenda primary.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa umma, hata kama ukimhamisha kutoka kituo ‘A’ kwenda ‘B’….

T A A R I F A . . .

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati yetu ni Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii ila hiyo ni a.k.a. (alias known as). (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine linalochanganya pia ni huku huku kuendelea kupotoshwa au kauli tatanishi. Leo hii Serikali ilisema kwamba hakuna kurudisha watoto shule za msingi mpaka sekondari, lakini leo hii hii Serikali inasema hakuna kukaririsha. Hivi tuelewe lipi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tukirudi tena kwenye suala lingine la hizi hizi kauli, Waraka wa Elimu Namba Tatu wa mwaka 2006 umetamka wazi majukumu ya kila mdau wa elimu kuanzia wazazi, Wakuu wa Mikoa hadi na walimu, lakini leo hii Mheshimiwa Rais anasema mzazi asihusishwe kwa mchango wa aina yoyote. Sasa je, hii michango ambayo inapaswa itolewe na wazazi au Serikali inaposema elimu bure, hii ni elimu bure au elimu bila ada? Tunaomba majibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia point nyingine kwamba sababu nyingine zinazochangia kuwepo kwa udororaji wa elimu ni kutolipwa kwa madai ya walimu kutokana na vigezo mbalimbali mara uhakiki wa watumishi hewa, mara uhakiki wa wenye vyeti fake, sasa tunataka tujue huu uhakiki wa wenye vyeti fake na watumishi hewa utaisha lini ili hawa walimu waweze kulipwa madeni yao mbalimbali kama madeni ya uhamisho, madeni ya kupanda madaraja nauli na vitu mbalimbali? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niendelee kuhusu uendeshaji wa shule za private. Shule hizi hazipo kwa kuwa tu eti zimejiamulia zenyewe. Shule hizi za private zimeanzishwa kwa kufuata kanuni na taratibu mbalimbali mojawapo ikiwa ni kupata usajili toka Serikalini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii Serikali imeanza kuziingilia hizi shule. Shule hizi zimewekeza, zinalipa ada na mzazi mwenyewe ameguswa, hakuangalia gharama, hakuangalia masharti mbalimbali akaamua kupeleka mtoto kwa matakwa yake yeye mwenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii shule za private wanaambiwa wasikaririshe watoto. Wakati mwanzo walipewa masharti na wakakubali na Serikali ikawapa usajili, lakini leo hii haieleweki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka nijue, hii Serikali ina mpango wa kuturudisha kule kwenye idadi ya kuongeza division four na tukose division one au two...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)