Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba na mimi niweze kuchangia, lakini naomba niseme kwamba nitachangia hii kamati Utawala na Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita sana kwenye suala la utawala bora. Taifa letu kwa mara ya kwanza tumeshuhudia kwamba hakuna Utawala Bora katika Taifa letu. Wapo viongozi walipandishwa vyeo baada ya kutuhumia na rushwa, kwa mfano aliyekuwa DC pale Arumeru na leo ni RC Mkoa wa Manyara, amepandishwa cheo licha ya kwamba alituhumiwa kwa rushwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushahidi ulipelekwa TAKUKURU, viongozi wetu...

T A A R I F A . . .

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mwingine kulumbana na watu ambao kwanza hawajui mambo ya nchi yanavyokwenda, siwezi kulumbana naye ngoja nimuache tu, wakati mwingine acha wafu wazikane wao wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiongozi anatuhumiwa kwa rushwa, ushahidi umeshapelekwa, Mbunge Nassari amepeleka ushahidi pale TAKUKURU, TAKUKURU wanachunguza anakuja kupandishwa cheo anakuwa RC. Hiki ni kitu kibaya sana katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, utawala bora katika taifa letu umekuwa ni msiba mkubwa sana. Leo tutakumbuka aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe alituhumiwa tena jukwaani na Paul Makonda ,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, yule bwana kaachishwa kazi, kwa sababu ya kutuhumiwa tu. Leo mtu alikuwa DC ushahidi upo umepelekwa TAKUKURU muda haujafika si mrefu anapandishwa kuwa Mkuu wa Mkoa. Taifa hili hakuna utawala bora na awamu hii utawala bora uko likizo na jambo hili hatuwezi kulivumilia hata kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu bomoa bomoa isiyofuta sheria. Leo wote tunafahamu kwamba kaya zaidi ya 1000 zilibomolewa pale Dar es Salaam, lakini kaya hizi zimebomolewa wakati kesi iko mahakamani. Leo mahakama inadharauliwa na mhimili mwingine, huu hauwezi kuwa ni utawala bora na tuheshimu mihimili hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wamekopa fedha benki, kuna watu ambao wamefariki kwa sababu nyumba zao zimesha bomolewa, hawana mahali pa kuishi, Taifa hili linaenaelekea wapi? Awamu ya Tano imetufikisha pabaya sana kwenye utawala bora, hatujawahi kushuhudia haya siku za nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nikuhusu kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa. Unapozuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa na nikopongeze sana Mwenyekiti, hii katiba, wewe Mwenyekiti kipindi hicho ulikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali hii; ukisoma Ibara ya Tatu ya katiba yetu Ibara ya Tatu Ibara Ndogo ya Kwanza inasema; “3.-(1) Jamhuri ya Muungano ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa, isiyokuwa na dini, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa.” (Makofi)

Mheshimiwa mwenyekiti, ukisoma pia Sheria Namba Tano ya mwaka 1992 ya vyama vya siasa inazungumzia shughuli ya vyama vya siasa ni pamoja na kufanya mikutano ya hadhara. Leo Rais wa nchi amezuia mikutano ya hadhara, ameikanyaga kanyaga Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ameiweka pembeni. Hakuna utawala bora, kama unaweza leo ukaweka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania pembeni. Hali hii ni mbaya sana hatuwezi kuivumilia. Na niombe viongozi tulio…

T A A R I F A . . .

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kufungia vyombo vya habari vinavyoikosoa Serikali. Leo vyombo vya habari vinafungiwa, tumeona magazeti yanafungiwa, gazeti la Mwanahalisi limefungiwa, Raia Mwema imefunguwa, Tanzania Daima ilifungiwa, utawala bora uko wapi? Kama leo vyombo vya habari vinavyoikosoa Serikali, vinavyoishauri Serikali, vinafungiwa, Taifa hili liko pabaya zaidi kwenye suala la utawa bora. Leo Bunge Live limefungiwa, hakuna Bunge live wote tunafahamu kwamba Bunge ni mkutano wa hadhara.