Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE.KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza mimi nimshukuru Mwenyezi Mungu pia kwa kunijalia kupata fursa hii ili kuchangia hoja tatu hizi zilizoko mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mjumbe wa Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa. Kwa sababu ya muda nitaomba nijikite katika taarifa hii/katika hoja hii ya Kamati yangu na nitakwenda kidogo tu kuchangia habari ya Mfuko Maalum huu wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfuko huu wa TASAF hapana ubishi kwamba umewakomboa wanyonge wengi kwa Serikali ya Muungano pamoja na Serikali ya Zanzibar. Mfuko huu umesababisha kuwapatia wale watu wa Kaya ya masikini walau milo yao mitatu kwa siku, lakini pia imewezesha watoto kwenda shule, lakini pia kwenda clinic. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata katika ripoti yetu katika kamati yetu imekuwa ikieleza mara kwa mara kwamba Zanzibar mfuko huu umekuwa ukifanya vizuri kuliko hata Tanzania Bara. Na kama Wajumbe sisi tulipata fursa mara nyingi tu kutembelea sehemu mbalimbali na mashuhuda wakawa wametoa ushahidi kuonekana kwamba mfuko huu umewasaidia sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo kidogo ambalo ni dosari na nilitaka Mheshimiwa Waziri wetu aweze kulijua, kwamba Zanzibar mfuko huu upo, lakini ni kama vile makao makuu unapeleka pesa kule lakini hawafuatilii utelekezaji wake mzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, tulipata fursa ya kutembelea Shehia moja ya Kilindi iliyoko Wilaya ya Chake Chake, Mkoa wa Kusini Pemba. Pale wananchi wenyewe waliibua mradi wa kuzuia maji ya bahari yasiingie katika mashamba yao na mradi ule ukakubaliwa na ukatengewa pesa za kutosha. Hata hivyo jambo la kusikitisha na haitakiwi maana si lazima uwe mchunguzi wa kada ya CAG ndipo uweze kuweza kujua value for money pale. Tuta lile lilikuwa na urefu wa mita 125; lakini tuliambiwa limejengwa kwa shilingi milioni 47. Kwa hesabu za haraka haraka unaweza kuona kila mita moja, basi imejengwa kwa zaidi ya shilingi 350,000. Sasa hapo unaweza kuona tu kama value for money haiwezi kupatikana hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiondoka hapo, sisi kama Wabunge, mimi kwa bahati nzuri pia katika shehia yangu ambayo imo katika jimbo langu na ndiyo shehia mimi mwenyewe naishi hapo kuna mradi kama huo wa tuta la kuzuia maji ya bahari yasiingie katika makonde/mashamba ya watu, lakini mimi kama Mbunge sijawahi kushirikishwa wala kuambiwa kama kuna mradi kama huo. Kwa hiyo, tungeomba walau na sisi tukapata fursa ya kushirikishwa tukajua miradi ambayo ipo katika shehia zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine ambalo limenikwaza sana, kama nilivyosema mwanzo miradi hii ikifika Zanzibar labda haina uangalizi mzuri. Tulikwenda tukatembelea ujenzi wa shule ya sekondari Muyuni mwaka jana. Shule ile ilijengwa hafla sana na takribani kwa zaidi shilingi 120, lakiniā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)