Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii nichangie hoja zilizoletwa na Kamati yangu ya Katiba na Sheria na Sheria Ndogo. Naomba nianze na Kamati yangu ya Katiba na Sheria naomba nimpongeze Mheshimiwa Jenista Mhagama, Waziri pamoja na watendaji wake wote kwa jinsi alivyoshirikiana na sisi kwenye Kamati yetu na kuweza kutuwezesha sisi kufanya kazi yetu vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ila ninayo maoni machache ambayo ningeomba kuyachangia. Nilikuwa naomba Kitengo cha Maafa kilichoko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu Serikali ijaribu kukiongezea fungu ili kiweze kuwafundisha wataalam mbalimbali wa maafa mbalimbali kama vile kuogelea (divers). Tunayo mifano mingi sipendi kukumbushia mambo ya zamani lakini tuliwahi kupata matatizo huko nyuma meli ya MV Bukoba ilipozama ilikaa chini kule muda kama wa wiki moja nafikiri kama tungekuwa na divers wazuri wale watu wangeweza kuokolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa naomba kitengo hiki kiongezewe nguvu na ikiwezekana zile sehemu zenye maziwa kama vile Ziwa Victoria, Nyasa, Tanganyika hao divers wawe based kule na pia kingeweza kufundisha wataalam wa zimamoto. Hilo ndio lilikuwa ni ombi langu kwenye Kitengo cha Maafa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo napenda niende ukurasa wa 14 wa wasilisho la Kamati ya Katiba na Sheria. Niipongeze Bodi mpya ya NSSF kwanza kwa kulichukulia suala na kuwasimamisha kazi wale wote waliofanya ubadhirifu pale NSSF. Lakini sasa niombe hatua zaidi zichukuliwe kwa sababu kumsimamisha mtu kazi tu haitoshi na kwa sababu pia tunayo Mahakama ya Wahujumu Uchumi, Mahakama ya Mafisadi ambayo imeanzishwa lakini haina kesi, itakuwa ni vizuri kama watu hawa wakapelekwa kwenye hiyo mahakama ili iweze kujulikana kama kwamba walifanya huo ubadhirifu au hawakufanya. Na ukiangalia Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipengele namba 107 kinatuambia kwamba mahakama ndio mamlaka ya mwisho ya utoaji haki. Kwa hiyo, kwa kuwapeleka mahakamani haki itatendeka itajulikana kama walifanya ubadhirifu au hawakufanya huo ubadhirifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kuongelea suala la The Law Reform Commission ambayo iko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Kamishna hii ipo lakini cha kushangaza zipo sheria nyingi nyingi ambazo zina matatizo hazibadilishwi kwa mfano Sheria ya Traffic, hii sheria bado ina faini za miaka ya nyuma sana ambayo iliachwa na wakoloni wetu watawala wetu. Kwa mfano, sheria hiyo ya traffic unaweza ukakuta mtu anagonga gari lakini anapokwenda mahakamani pale akikiri kosa faini ya mwisho ni shilingi 50,000.

Mimi nadhani hii kamisheni ingefanya kazi yake ili iweze kuzichukua zile sheria zote ambazo zina matatizo iweze kuzirekebisha kwa sababu inawezekana wakati wanazitunga zilikuwa zinafaa wakati huo kuwa na faini ya aina hiyo lakini sasa miaka mingi ilikwishapita na nchi zimeendelea na mambo yamekuja mengi. Sasa huwezi ukakaa na faini ambayo imetungwa toka mwaka 1963 bado unatoza faini hiyo hiyo. Nilikuwa naomba hiyo sheria iweze kurekebisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine hii kamisheni nilikuwa naomba ijaribu kurekebisha sheria…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.