Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, imekuwa ikisemwa mara nyingi kuwa kilimo ni uti wa mgongo wa Taifa letu na 75% ya ajira inapatikana katika kilimo na 100% ya chakula Tanzania inatokana na kilimo lakini Serikali bado haijawekeza katika kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa 80% ya wakulima wetu wanatumia jembe la mkono ambapo mazao yanayopatikana ni machache ukilinganisha na wakulima wanaotumia zana bora na za kisasa katika nchi za wenzetu. Hivyo inahitajika Serikali yetu iwekeze katika kilimo kwa kuwapatia wakulima zana bora za kisasa na pembejeo na kuwapatia mikopo yenye masharti nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Serikali ianzishe utaratibu wa kuwalipa fidia wakulima pale inapotokea majanga kama ukame, wadudu/wanyama waharibifu, mafuriko au mvua zinazoangamiza mimea mfano mvua za mawe na bei inaposhuka. Kwa kufanya hivi itawasaidia wakulima kupunguza hasara wanayopata kutokana na majanga haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, Serikali iweke matawi ya benki katika kila wilaya ambazo zinajishughulisha na kilimo. Kwa mfano, katika Jiji la Tanga ziwekwe benki katika maeneo yenye wakulima na wafugaji kama Kata za Tongoni, Kirare, Mzizima, Mabokweni, Chongoleani na Kiomoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, kilimo cha umwagiliaji. Katika miradi ya kilimo cha umwagiliaji (irrigation schemes) imekuwa ikifanya kazi pale inaposimamiwa na wafadhili lakini wafadhili wakiondoka tu, miradi hii yote inakufa au kuwa na hali mbaya. Serikali iangalie kwa umakini miradi hii kwa kuitengea fedha za kutosha ili hata pale wanapoondoka wafadhili, miradi hii iendelee kuwa na tija na faida kwa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tano, maji ni uhai na ni nyenzo muhimu katika shughuli za maendeleo kama kilimo, lakini hata mashine nazo zinahitaji maji. Miradi ya maji vijiji 10 kila Halmashauri inakwenda kwa kusuasua, fedha za miradi zinacheleweshwa sana na ni kidogo. Wito wangu ni kama ifuatavyo:-

(i) Serikali ipeleke fedha kwa wakati;

(ii) Katika miradi ya maji ipite/itumie Mamlaka za Maji zilizopo kwa kuwa wanaweka mitambo ya maji kwa uzoefu waliokuwa nao na wanategemea mtandao wa maji kama chanzo chao cha mapato kila mwezi kwa kupitia bili za kila mwezi; na

(iii) Serikali ianzishe miradi ya visima virefu na vifupi katika maeneo yenye ukosefu wa maji hususani katika vijiji ambavyo havikubahatika kupitiwa na miradi ya maji vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sita, uvuvi ni sekta ambayo imeajiri Watanzania wengi katika maeneo/mikoa yenye maziwa na bahari. Tanzania ina ukanda mrefu wa bahari kilometa 1,425 kutoka Jasini, Wilaya ya Mkinga, Mkoa wa Tanga. Wavuvi hawaelimishwi juu ya uvuvi bora na wa kisasa bali mara kwa mara wavuvi wanasulubiwa kwa kisingizio cha uvuvi haramu, wananyang’anywa mashua na majahazi, nyavu na vifaa vingine vya uvuvi na vinatangaziwa kuharibiwa/kuangamizwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vifaa kama nyavu vinatengenezwa katika viwanda vya hapa nchini na pia vinaingizwa kupitia mipaka na bandari zetu na Serikali inakusanya kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika sekta hii nashauri mambo yafuatayo:-

(i) Serikali itoe elimu kwa wavuvi juu ya nyavu zinazofaa na ipige marufuku nyavu zisizohitajika kuingizwa nchini;
(ii) Serikali isiangamize/kukamata wavuvi na mali zao na kufanya replacement ya vifaa haramu dhidi ya vifaa halali ili tusijenge uadui kati ya wavuvi dhidi ya Askari wa JWTZ na Coastal Zone;

(iii) Serikali ianzishe vipindi vya redio na televisheni kutoa elimu ya uvuvi na mazingira; na

(iv) Serikali ianzishe Benki ya Wavuvi kama ilivyo Benki za Wakulima.