Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu umuhimu wa Sekta ya Kilimo ambapo zaidi asilimia 57 ya wananchi wa Tanzania wanalima na kufuga na pia katika suala la ukuaji wa uchumi kwa mazao ya biashara na chakula, mfano zao la korosho ambalo leo Tanzania ni wanufaika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mchango wa kilimo katika Taifa hili kwa zaidi ya asilimia 28 katika pato la Taifa, lakini leo wakulima bado hawapati faida na mazao yao na hivyo wanufaika wakubwa wamekuwa wafanyabiashara wa mazao zaidi ya wakulima maskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itaweka mifumo mizuri ili wakulima nao wafaidike na mazao yao nchini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na juhudi za Serikali kusambaza mbolea mikoani, lakini bado imeshindwa kwa asilimia kubwa kusambaza kwa wakati. Kwanza mbolea inasambazwa kwa kuchelewa na ikifika, wakulima wanapata mbolea wakati tayari kipindi cha kuweka mbolea kwenye mazao kimepita? Je, Serikali haioni kwamba kila mwaka inashindwa kusambaza mbolea? Nini mkakati wa kusaidia jambo hili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, mbolea zinafika chache kwa wakulima. Tatu, bei ya mbolea ni kubwa sana, wananchi maskini ambao ni wakulima wa mikoani (vijijini) wanashindwa kununua mbolea hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, natumizi na elimu kuhusu mbolea hizi zinazotolewa, lakini ni lini wakulima watapatiwa elimu ya kutosha ili wapate mazao mengi na faida? Lingine ni mfumo wa ugawaji mbolea, pia una urasimu mkubwa; lini utakwisha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikoa iliyopakana na nchi jirani kuna hili tatizo la mbolea fake. Mfano Mikoa ya Mbeya, Katavi na Kigoma. Ni lini Serikali itasimamia mbolea fake inayopita mipakani ili kusaidia wakulima ambao wengi wao wananunua mbolea fake hizi ambazo ni bei rahisi? Nini Tamko la Serikali katika jambo hilo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Katavi Jimbo la Nsimbo, Mpanda Mjini na Tanganyika ni maeneo ambayo tumbaku inalimwa, lakini bei ya tumbaku kwa wakulima hawa ni ya dhuluma. Walanguzi wamekuwa wakipanga bei wao na kuacha wakulima maskini hawapati faida. Nini tamko la Serikali kuhusiana na wizi huu wa bei ya zao la tumbaku unaofanywa na walanguzi wasio waaminifu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni migogoro ya wakulima na wafugaji katika maeneo mbalimbali nchini; ni kwa nini Serikali inashindwa kutenga maeneo ya malisho nchini ili kupunguza kesi katika Mahakama kwa migogoro hii mikubwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia maoni ya ushauri wa Kamati, nashauri Serikali itenge maeneo ya malisho ili kuondoa malalamiko ya wafugaji; ng’ombe zao kupigwa risasi zikiingia kimakosa hifadhini, mfano, Kata ya Majimoto, Luhafwe na Ikuba. Je, ni kwa nini Askari wa Wanyamapori wanapiga risasi ng’ombe kwa maelekezo ya Wakuu wa Mikoa na Wilaya? Ni lini Serikali itaacha uonevu huu kwa kushindwa kutatua matatizo haya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Ziwa Tanganyika zoezi la kudhibiti uvuvi haramu katika ziwa hili, limesababisha uonevu mkubwa kwa wananchi. Ni kwa nini hamwoni haja ya Serikali kuwapatia nyavu zenye bei rahisi kwa mikopo katika vikundi vyao na kuwasimamia ili kudhibiti uvuvi haramu na siyo kufanya zoezi la kudhibiti uvuvi haramu huku wavuvi hawajiwezi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo hakiwezi kutegemea mvua tu. Naomba Serikali ipitie bajeti yake kwa upya na kuhakikisha inaharakisha kumaliza miradi ya maji kwa muda muafaka. Vile vile nashauri Serikali iendelee kutekeleza miradi hii kwani Serikali inapata hasara na wakulima hawapati faida.