Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono taarifa ya Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji. Naomba kuchangia katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ni vyema Serikali (Wizara ikawa inatoa fedha zote zinazoidhinishwa na Bunge, kuliko ilivyo sasa, fedha kidogo inayotolewa na Serikali katika hizi Wizara ambazo zinatoa ajira kubwa kwa Watanzania. Pia nashauri Serikali iongeze bajeti katika Wizara hizi tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imekuwa kawaida ya Serikali kutotekeleza ushauri na maagizo yanayotolewa na Bunge lako Tukufu kila mwaka, kwani mapendekezo yamekuwa yanajirudia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni mbolea kutofika kwa wakati. Vile vile kutokuanza kwa uzalishaji wa mbolea katika viwanda vyetu viwili vya Kilwa na Mtwara pamoja na malighafi tuliyonayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu Benki ya Maendeleo ya Kilimo kuongezewa mtaji na kufungua matawi kwenye maeneo ya kilimo kuliko hivi sasa kwamba matawi mengi yako Mjini. Pia Mheshimiwa Waziri wa Kilimo apewe nafasi kubwa katika kuendesha benki hii kuliko ilivyo sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuongeza tozo kwenye Mfuko wa Maji hadi Sh.100/= kwa lita ya petroli na dizeli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kuwe na mahusiano kati ya Wizara ndani ya Serikali ili kutekeleza dhana ya mapinduzi ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni uvuvi. Hapa pana ajira kubwa, Serikali inatakiwa kuacha tabia ya kuharibu zana za wananchi wanyonge badala yake ishughulike na viwanda.