Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pembejeo kulingana na changamoto hii, imekuwa ikiwaathiri wakulima wengi kulingana na changamoto ya bei ya pembejeo yenyewe, upatikanaji wake, kwani suala hili linawaathiri sana wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kilimo cha umwagiliaji; pesa nyingi zimepotea katika mabwawa. Suala hili haliwezi kufanikiwa, kwa sababu bado ni changamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la utafiti ni muhimu sana ili tuweze kuinua kilimo chetu kuwa chenye tija kwa kuwa utakuwa umefanyika utafiti kuwa wapi panafaa na panafaa kwa kilimo gani katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la soko limekuwa changamoto kubwa kwa wakulima wengi nchini ikiwemo watu wa Mkoa wa Rukwa ambao wanalima mazao ya chakula, lakini Serikali ilitoa tamko au katazo juu ya wakulima kuuza mazao yao nje ya nchi wakati huo Serikali imeshindwa kuwatafutia soko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetoa bei elekezi kwa mbolea zinazopelekwa mikoani ikiwemo Mkoa wa Rukwa. Suala hili limeshindwa kutekelezeka kwani suala la barabara limekuwa linachangia bei elekezi, haitawezekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na uzoefu ambao tumekuwa nao, suala la wakulima wetu kusubiri msimu wa kilimo, ni vyema Serikali ikajenga mazingira rafiki kwa wakulima kuwa na kilimo cha umwagiliaji.