Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kutoa bei elekezi kwa wakulima wakati pembejeo zinauzwa kwa bei ya juu mfano, mbolea ya DAP Sh.60,000/= na Urea ni Sh.50,000/= siyo sahihi kabisa. Wananchi wamehamasishwa kulima mazao mbalimbali lakini bei za mazao hayo iko chini sana. Mahindi yanauzwa hadi Sh.3,000/= mpaka Sh.5,000/= kwa debe. Kwa kweli hii inasikitisha sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ione ni namna gani itawatafutia soko la uhakika la mahindi na mbaazi na kushusha bei ya pembejeo.

Mheshimiwa Spika, kilimo ni uti wa mgongo na asilimia 75 ya Watanzania ni wakulima, lakini Wizara hii haipewi bajeti ya kutosha itakayosaidia kuleta pembejeo za kutosha na kwa wakati. Naiomba sana Serikali itenge bajeti ya kutosha na kuitoa kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kumekuwa na migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji, naiomba Serikali ione ni namna gani inatenga maeneo ya wakulima na wafugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna ng’ombe wanazagaa ovyo ovyo kwenye maeneo ya wakulima, watu wamekuwa wakiuana. Naishauri Serikali ifanye haraka kutenga maeneo, mfano nimeshuhudia wakulima na wafugaji wanapigana pale Njombe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.