Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. ZAINABU M. AMIRI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa kipindi cha Januari, 2017 mpaka Januari, 2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni yangu. Ili kutekeleza kwa vitendo Maoni na Mapendekezo ya Kamati, Serikali itoe bajeti ya kutosha ili itumike kwa muda sahihi kuweza kutekeleza mambo yote yanayojadiliwa na kupendekezwa katika Kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ijenge na iboreshe maghala ili kuweza kuhifadhi mazao ya nafaka sehemu salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iongeze viwanda vya pembejeo za kilimo, madawa na mbolea nchini ili wakulima waweze kupata zana hizo kwa wakati na kuvitumia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kutoharibu vifaa vya uvuvi mfano ngalawa ambazo si zana haramu katika uvuvi; hivyo visiharibiwe.