Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchukua fursa hii kuchangia taarifa nzuri ya Kamati na kushauri kuboresha katika maeneo mbalimbali kwa kila sekta.

Kwanza, nishauri suala la mbolea, bado tozo ya USD 10,000 kwa mbolea mpya ingeondolewa na Serikali, hii imefanya aina nyingi za mbolea hasa za maji kwa ajili ya (horticulture) kilimo cha mbogamboga na matunda kukosekana sokoni. Pia Serikali iangalie jinsi ya makampuni za mbolea zitoe huduma za ugani (soil testing) kupima udongo badala ya kuiachia Serikali kama Zambia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri tuwekeze kwenye utafiti, zaidi kwenye mbegu ambapo asilimia 75 za mbegu za mahindi zinatoka nje ya nchi, mbegu za mazao ya kahawa mafuta kama alizeti, soya na mbogamboga asilimia 95 zinatoka nje ya nchi. Tuna uwezo wa kuzalisha mbegu zetu nchini, pia hulinda viwanda vyetu vya mbolea na mbegu zinatozwa kodi, tozo, ushuru na ada mbalimbali tofauti zinazoingizwa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri Serikali iweke bajeti ya kutosha kuboresha vituo vyetu 16 vya kilimo kwa kuongeza vifaa vya kazi na nyenzo mbalimbali. Makutupora wamalizie kuwekeza katika vifaa vya tissue culture, tuwekeze kusindika mazao yetu nchini badala ya kusafirisha mazao ghafi kama korosho, kahawa, pamba mbaazi mikunde na kadhalika. Serikali kupitia ASA na vituo vya utafiti, wapewe bajeti ya kuagiza miche ya matunda ambayo tunaweza kuzalisha nchini kama (apple, peas, plums, citrus, grapes) hata jamii ya michungwa, embe, nanasi, zabibu zikiletwa chache, tutazalisha nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iondoe au kupunguza kodi, tozo, ushuru na ada nyingine katika sekta ya kilimo ikiwemo kodi ya ardhi, malimbikizo makubwa mfano; ni VAT, Income Tax, Withholding Tax, Land Rent, OSHA, Fire Rescue, TBS, TFDA, Weights and Measurements, WCF na nyingine nyingi, uzalishaji nchini inakuwa gharama kuliko kuagiza kutoka nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaishauri Serikali kuondoa kodi kwenye kuagiza (Importation) kwa mitambo ya kuchimba maji (Borehole drilling equipment) pamoja na mitambo ya kuchimba mabwawa ya kuvunia maji (Excavators, Bulldozers, Shovels Rollers) itasaidia kupunguza gharama za uchimbaji visima na mabwawa kama ushindani utakuwepo kutokana na mitambo kuwa mingi. Tutoze kodi kwenye kazi na siyo Importation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nasisitiza iongezwa Sh.50 kwa maji vijijini na kuundwa kwa Wakala wa Maji Vijijini. Nashauri tuondoe kodi ya pampu za sola za maji (Solar water pump) ili kuondoa adha ya akinamama kuchota maji mbali na makazi yao pamoja na kupunguza gharama za kusukuma maji kwa kutumia mafuta ya diesel na umeme kwa miradi midogo ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ugani wa madawa ya mimea na mifugo pia zitolewe na makampuni yanayouza hayo madawa. Serikali iondoe kodi kwenye madawa, chanjo vifaa tiba vya mifugo na chakula cha mifugo (Supplements) na kurudisha VAT kwenye chanzo cha mifugo ili waweze kupata unafuu wa kupata taxes.