Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. ZAINAB M. AMIRI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa taarifa ya 2017 – 2018 Januari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itenge bajeti ya kutosha ili kuwezesha sekta ya utalii, maliasili na ardhi iweze kuwekeza kwa muda muafaka, hatimaye kuweza kuingizia Pato la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itoe elimu ya kutosha kwa wananchi wetu ili kuweza kutunza mazingira yetu ili yasiharibike na hususan ndani ya hifadhi zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iwekeze vya kutosha kutangaza vivutio tulivyonavyo nchini kwetu, si kwa mbuga za wanyama na Mlima Kilimanjaro tu bali hata vivutio vingine kama Mapango ya Amboni na kadhalika ili kuweza kuliletea pato Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ijenge utaratibu wa kutatua migogoro ya ardhi kwa wakati ili kuweza kulimaliza tatizo hili na wananchi waendelee na shughuli za uchumi na uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhakiki mashamba (makubwa) yaliyotelekezwa ili kuyabaini na Serikali kutoa ardhi hiyo kwa wananchi waliokosa ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Hifadhi la Wanyamapori wawe na utaratibu wa kutoa fidia kwa wananchi ambao watajeruhiwa au kuuawa na wanyamapori.