Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Nianze na suala la maji. Naiomba sana Serikali, Wizara ya Maji, Mamlaka za Maji, zinazidai taasisi za Serikali pesa nyingi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninazungumza hivi, lazima Mheshimiwa Waziri wa Fedha atufahamu. Taasisi za Serikali zinadaiwa fedha nyingi sana kiasi kwamba Mamlaka zetu za Maji zinafika wakati zinashindwa kujiendesha. Naomba sana Serikali iweze kulipa madeni yale. Ikilipa madeni yale kuna hizi Mamlaka za Maji zitaweza kujiendesha zenyewe bila kutegemea ruzuku kutoka Serikalini. Kwa hili namuomba sana Mheshimiwa Waziri na Serikali iweze kusimamia tatizo hili kuhakikisha taasisi zetu za Serikali zinalipa madeni ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliahidi kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi tutamtua mama ndoo ya maji, sasa leo twende katika hali ile. Mheshimiwa Waziri…

T A A R I F A . . .

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeipokea Taarifa kwa mikono miwili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, sisi kama Wabunge, ndio wananchi. Hawawezi kuja wananchi wote ndani ya Bunge hili kuja kuchangia ndani ya Bunge hili, halitoshi. Tumeishauri Serikali mara nyingi iongeze shilingi 50 ifike shilingi 100 kwenye petroli na dizeli ili tukaokoe matatizo ya maji vijijini na mijini. Nashangaa sana Serikali hii haitaki kutusikiliza sisi Wabunge. Sisi ndio tunaokaa na wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuomba sana, naiomba Wizara iweze kutusikiliza sisi Wabunge. Sisi ndio wananchi wenyewe tunaokuja hapa, Mheshimiwa Waziri wa Fedha, wewe sio peke yako. Naomba sana kwa hili Serikali iweze kulifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni la uvuvi. Suala la uvuvi namwomba sana Mheshimiwa Waziri, uvuvi tunao mkubwa sana katika bahari. Namwomba Mheshimiwa Waziri tena, uweze kuelekeza macho yako katika bahari. Tunaweza kukuza uchumi mkubwa katika nchi yetu. Mheshimiwa Waziri, kuna nchi nyingi sana zinategemea uvuvi wa bahari kuendeleza katika kipato cha nchi yao, lakini Mheshimiwa Waziri tunashangaa Serikali yetu, tatizo tumeshazungumza mara nyingi la kupatikana bandari ya uvuvi, hakuna; kupatikana meli za uvuvi hakuna… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)