Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kusema naunga mkono taarifa zote mbili na maazimio yake. Pia nawapongeza Wenyeviti wa Kamati hizi kwa kazi nzuri waliyofanya pamoja na Wajumbe wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda, niende moja kwa moja. Nilitaka nichangie kwenye eneo moja la mahusiano yaliyopo kati ya wafugaji na hifadhi zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa takwimu zilizopo, kwa nchi za Ukanda wa Kusini huku na Afrika Mashariki, Tanzania ni nchi inayoongoza kwa kuwa na mifugo mingi. Inasemekana tuna zaidi ya ng’ombe 28,000,000 na pointi zake, lakini pia kuna mbuzi, kondoo na mifugo mingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa takwimu, sekta hii ya mifugo inasemekana inahudumia zaidi ya kaya 4,000,000 ambazo zinajumlisha zaidi ya watu 25,000,000 ambao ni karibia zaidi ya asilimia 50 ya population ya nchi yetu. Kwa takwimu hizo hizo, sekta hii ya mifugo inachangia zaidi ya 4% kwenye pato la Taifa ambalo inashindana karibu sawa na madini katika nchi yetu. Kwa hiyo, ni sekta kubwa na inagusa eneo kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali inayoendelea kwenye sekta hii ya mifugo ni mbaya sana. Bahati mbaya kwa miaka sasa hili jambo limekuwa linakuja, linazungumzwa hapa Bungeni, moto unawaka, halafu zinachukuliwa hatua za kuufunika ule moto, watu wananyamaza, halafu dhuluma na hujuma inaendelea pale pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2013/2015 moja ya kazi nilizofanya ni pamoja na kupita kwa wafugaji nchi nzima, kuwasikiliza na kusikia manung’uniko yao. Nilitegema baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 hali itabadilika. Bahati mbaya sana, juzi nikiwa Mjumbe wa Kamati hiiya Ardhi, Maliasili na Utalii, tumekutana na wafugaji walikuja hapa Dodoma, hali ni mbaya kuliko ilivyokuwa mwanzo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tutaendelea na hatua hizi za kuzima moto kila unapowaka, maana yake ni moja, tunatoa kafara asilimia 50 ya population ya nchi yetu ambayo inahudumiwa na sekta ya mifugo na kuacha hali yao ikiwa mbaya sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tunavyoongea na hapa nataka niijenge hii hoja tuuunge mkono pendekezo la Kamati la kuunda Kamati Teule ya Bunge kwenda kusaidia kumaliza tatizo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu kwa hatua za kawaida za Serikali, tukubali imeshindikana. Njia peke yake iliyobaki, tuunde Kamati Teule ya Bunge ikaisaidie Serikali kwa nia njema ya kuokoa zaidi ya asilimia 50 a population ya nchi yetu ambayo inahudumiwa na sekta hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi tunavyoongea mifugo ambayo imeshikiliwa kwenye hifadhi kwa takwimu hizi kama ni za kweli, basi hali mbaya sana. Meatu kuna ng’ombe 948; Kakonko ng’ombe 700; Bukombe ng’ombe 716; Bariadi 158; Kasulu 90; Morogoro 401; Chemba 411; Mlele 640 na Kaliua ng’ombe 1,129; hawa wameshikiliwa kwenye hifadhi. Wapo wanaoendelea kufa kwa sababu hawana huduma za kutosha, wapo wanaouzwa kinyemela na wapo wanaouawa kwa risasi. Hali hii ikiendelea tunakokwenda ni kubaya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa takwimu nilizonazo mwaka 2015 - 2018 ng’ombe ambao wameshauawa kwa kupigwa risasi na wengine kwa kunyimwa huduma, kwa sababu wako wengi ambao wamekamatwa, namna ya kuwahudumia ni ngumu, Katavi ng’ombe 6,503; Morogoro Vijijini ng’ombe 200; Bunda ng’ombe 150; Meatu ng’ombe 48; Chemba ng’ombe 196; hii ni mifano ya maeneo machache. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa…

(Hapa kengele ililila kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)