Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwapongeza Kamati ya Nishati na Madini kwa taarifa nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na utekelezaji mzuri wa miradi ya REA, naungana na Kamati kupendekeza kuwepo kwa usimamizi mzuri wa hii miradi ili iwe endelevu kitaalam. Usambazaji kwa maeneo ya vijijini, waya zinawekwa umbali mrefu na pia miundombinu ya nguzo za kawaida ni changamoto kutokana na mazingira ya vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kazi nzuri inayofanywa na REA, napendekeza Serikali iwe na mkakati wa kuimarisha wataalam wa TANESCO ili waendane na ongezeko na kasi ya usambazaji wa umeme kwa mpango wa REA. Kutokana na ongezeko la usambazaji wa umeme kumesababisha kuzorota kwa huduma za dharura (emergency) hasa katika maeneo ya vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.