Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kutoa mchango wangu. Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema nikaweza kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kutoa mchango huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na suala la REA, na katika hili suala la REA nianze kwa kuipongeza Serikali. Kupitia REA Serikali inafanya kazi nzuri ya kuwapelekea vijijini huduma hii muhimu katika maendeleo ya Watanzania. Pamoja na jitihada nzuri za kupeleka umeme vijijini kupitia REA, changamoto za REA ukiziangalia kwa kwa undani zinasababishwa na mambo makubwa mawili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza, mimi nipo kwenye Kamati ya Nishati na Madini, tumekuwa tukiishauri Serikali zile tozo za kutoka kwenye mafuta kwenda kwenye mfuko wa REA zimekuwa ring-fenced lakini kumekuwa kuna mkwamo, ile hela haiendi moja kwa moja kwenye mfuko ili iweze kwenda kwenye REA kuhudumia usambazaji wa umeme vijijini.

Kwa hiyo, nipende kuiomba Serikali wakati wanafanya wind up tusikie upande wa Serikali ni lini hii automation ya transfer ya hela, kwa sababu mwananchi akienda kununua mafuta kwenye sheli (Shell/Petrol Station) ile tozo inatozwa pale pale analipa cash, sasa kwanini kunakuwa kuna mkwamo? Kwa nini hii hela isiende moja kwa moja kwenye mfuko wa REA ili wakala wa REA waweze kusambaza umeme vijijini bila kusuasua? Pia kwenye REA hapo hapo kwa upande wa TANESCO ukiangalia TANESCO na REA wanavyofanya kazi ni sawa na treni ambayo ina mabehewa mengi lakini ina kichwa cha treni ambacho uwezo wa engine yake ni mdogo sana.

Mheshimiwa MNaibu Spika, kichwa cha engine ni upande wa TANESCO; TANESCO ina madeni makubwa imefika kwenye point ambapo inaweza ika-collapse kwa sababu inadaiwa na inashindwa kutoa huduma ya umeme nchini kwa sababu ya madeni makubwa zile cost za maintenance zimekuwa accumulative. Kwa hiyo, ile speed ya REA kusambaza umeme vijijini inakwamishwa na TANESCO kushindwa kufanya majukumu yake kwa sababu haina pesa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipendekeze Serikali ifike mahali idara zile za REA ambazo zinahusika na kusambaza umeme vijijini tuvi-merge na REA ili ule ufanisi wa REA zile idara ambazo zipo upande wa TANESCO ambazo zinahusika na huduma za umeme vijijini viwe-merged kwenye REA ili REA iendelee kufanya kazi vizuri kama inavyofanya; halafu TANESCO inayobaki iendelee kutoa huduma ya umeme maeneo ya mjini. Tukifanya hivyo wananchi wetu vijijini watapata umeme vizuri bila kusua sua na upande wa mijini TANESCO itajikita kutoa umeme mjini. Hii itatupeleka kwenye dhamira ya kwenda kwenye uchumi wa viwanda na kwenda kwenye uchumi wa kati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ambalo ningependa kulizungumza ni miradi mikubwa ambayo Watanzania wanaisubiri kwa hamu kubwa sana ya kutufikisha kwenye uchumi wa viwanda. Miradi hii ni pamoja na Mradi wa Stigler’s Gauge ambao ni mradi mkubwa sana. Ninamshukuru Rais Magufuli na Serikali ya Awamu ya Tano kwa kulisimamia hili. Mradi wa Standard Gauge Railway ni mradi mkubwa sana, Tanzania itakuwa kama Ulaya miradi hii ikitekelezwa. Hata hivyo sisi Bunge tunatakiwa tuwe sehemu ya kui-facilitate Serikali iweze kutekeleza miradi hii kwa kasi ya haraka sana kwa sababu Watanzania wanasubiri miradi hii kwa hamu kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nipende kupendekeza kwa mikopo ya nje ambayo inaweza ikawezesha Serikali kutekeleza miradi hii. Ifike mahali tuangalie mechanism ya Bunge ya kuwa na oversight kwa Serikali lakini bila kuikwamisha Serikali katika kuwa na wigo wa kwenda kukopa mikopo ya bei nafuu. Wakati tunajadili Kamati ya bajeti hapa kulikuwa kuna hoja kwamba kwa nini Serikali imekopa additional ya shilingi bilioni 1.46 kabla ya kuja Bungeni.

Sasa nipende kupendekeza kwamba Serikali mje na mechanism ambayo itatufanya sisi ile checks and balance yakuisimamia Serikali inakuwepo. Lakini Serikali bado mnakuwa na freedom pale fursa inapojitokeza ya kukaa na hizi Development Financial Institutions, kukaa na wale wanaoweza kutupa mikopo ya bei nafuu kwa ajili ya miradi ya bei nafuu kama Stigler’s Gauge na SGR muweze kufanya hivyo kwa sababu hakuna Serikali ambayo inadhamira ya njema na Watanzania kama Serikali ya Awamu ya Tano. Sasa kwanini tuwe sehemu ya kikwazo badala ya kui-facilitate ili iweze kutoa maendeleo ambayo tumewaahidi Watanzania kwa kasi ambayo Serikali inataka twende. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nichangie kuhusu upande wa sekta ya madini hasa hasa wachimbaji wa kati na wadogo. Kwa miaka mingi tumeona watu wanaochukua hizi Special Mining Licenses, tumehangaika nao, lakini kwa sababu ya uchanga wa sekta na taasisi zetu kuendelea kuzijengea uwezo tumekuwa na changamoto kubwa sana ya kupata fair share ya tax collection.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nipende kupendekeza kwamba Serikali ifike mahali jitihada zote tuzipeleke kwenye hawa wachimbaji wa kati ambao tukiweza kuwa-facilitate wataweza kutengeneza ajira humu humu nchini na pia yale mapato ambayo wanayapata yatawekezwa hapa hapa Tanzania, badala ya kuendelea kuangaika na ku-facilitate wawekezaji wakubwa wa Kimataifa ambao wanafanya tax planning, madini yetu yanaenda kodi hatuzioni, wanatuachia mapango tu kwenye nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naamini Serikali kwa sababu ipo katika ku-reform ili kuhakikisha resources za nchi zinawanufaisha Watanzania jambo hili nadhani limefika mahali pake. Tumetembea kwenye mikoa ambayo inachimba dhahabu wachimbaji wa kati wana uwezo mkubwa sana. Teknolojia za dunia sasa hivi zinaweza zikawa adopted na hawa wachimbaji wa kati wakaweza kuisimamima migodi vizuri lakini pia wakaajiri Watanzania na mapato wanayopata yanabaki hapa hapa nchini.

Kaka yangu Mheshimiwa Lubeleje ameniomba dakika chache nimuachie kwa hiyo naomba niishie hapo ili Mheshimiwa Lubeleje kaka yangu uweze kutumia hizo dakika. Nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.