Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Charles Muhangwa Kitwanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Vilevile nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa jinsi ambavyo amekuwa mwema pamoja na matatizo niliyopa sasa ni mzima kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu wa Spika, nianze kwanza kwa kuipongeza sana Serikali kwa uamuzi wake wa kuhakikisha kwamba inajenga miundombinu itakayowezesha uchumi wetu kupaa. Serikali imejikita katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na reli, tunakuwa na viwanja vya ndege, tunakuwa na barabara na tunakuwa na mashirika ambayo yanaweza kweli kweli kuonekana kwamba ni mashirika ambayo yana nia ya kuonesha kwamba tunajenga uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, na kikubwa ambacho nikiseme ni jinsi ambavyo Serikali imeweka kipaumbele kuhakikisha kwamba inatumia fedha zake za ndani. Hili nilisisitize kwa sababu kuna watu hapa wanasema kwamba kukopa si fedha za ndani. Hicho ni chanzo kingine katika kuhakikisha kwamba unajipatia pesa katika Serikali yako. Aidha, unaweza ukakusanya ushuru, unakusanya pesa na kupata revenue. Vilevile unaweza ukakopa ukapata hizo pesa na baadaye utalipa kwa kutumia pesa zako za ndani. Kwa hivyo kukopa ni pesa zako za ndani.

Mheshimiwa Naibu wa Spika, pamoja na pongezi hizo niangalie tu namna ambavyo tunaweza tukahakikisha kwamba uchumi wetu unapaa kwa haraka sana. La kwanza ni linkages. Tunapojenga reli, tunapopanua bandari ni lazima tuangalie ni kwa namna gani hiyo bandari itaweza kuharakisha uchumi wetu. Huwezi kuwa na bandari iliyo nzuri halafu mizigo inafika huna mahala pa kuiweka. Kwa hiyo, dry ports ziwekewe umuhimu unaolingana na jinsi ambavyo tunapanua bandari zetu, ikiwemo dry port ya pale Fela katika Jimbo la Misungwi.

Mheshimiwa Naibu wa Spika, vilevile niipongeze Serikali kwa kuweka umuhimu wa pekee katika kuhakikisha kwamba Shirika letu la Simu la TTCL linaimarishwa. Nizungumzie umuhimu uliopo kwa Shirika la TTCL na tuangalie ni kwa namna gani Serikali iliangalie shirika hili kwa umuhimu wa kipekee.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii tukiingia vitani Airtel wakaondoka, Vodacom wakaondoka na mashirika ya binafsi yakaondoka tutawasiliana vipi? Ni vyema tukaona huu umuhimu na tukaweka nguvu sahihi ya kuhakikisha kwamba Shirika letu la Simu la TTCL linapewa kila msaada na isiwe msaada tu wa pesa au vifaa kwa sababu matatizo mengine yanatokana na namna ya uendeshaji, na hili nitajaribu kulizungumzia na nitoa ushauri kwa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu wa Spika, ushauri wa kwanza ni kuhusu usimamizi na katika kusimamia niombe Serikali iangalie uwezekano wa kuwa na mfumo wa eyes on hands off. Serikali isiingilie ingilie haya mashirika hasa hasa yale ambayo Serikali imeya-own kwa asilimia kikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sioni kwa nini kama Serikali imejenga ikaweka bodi imara na bodi yenyewe ikaajiri Mkurugenzi au Mtendaji Mkuu imara, na kukawa na mfumo mzuri wa mawasiliano kila siku Katibu Mkuu au Waziri aende kuweka mkono wake kwenye shirika hilo. Yeye Waziri, Katibu Mkuu na Wizara mama ihangaike na kuhakikisha kwamba tuna sera zilizo sahihi na hizo sera zinajengewa mfumo wa utekelezaji na hao wajumbe wa Bodi pamoja na menejimenti yake kuweza kutekeleza ile sera ambayo Serikali ingependa itekelezwe.

Mheshimiwa Naibu wa Spika, vilevile kujengwe mahusiano mazuri ya mawasiliano. Sioni kwa nini kama menejimenti wanakaa kila wiki kwa vyovyote vile wataitaarifu bodi kinachoendelea labda kila quarter, lakini Bodi nayo iwajibike kumweleza Waziri na Katibu Mkuu nini kinachoendelea kwenye shirika hilo angalau kwa muda ambao watakuwa wamejipangia. Hapo kila mtu atakuwa ametekeleza wajibu wake yake bila kumwingilia mwingine. Tunaangalie vilevile nilikuwa nakizungumzi issue ya linkage, hii ni kitu muhimu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa unakuta tunahangaika kutengeneza reli, reli inapokuwa inajengwa kutoka Dar es salaam kuja Morogoro unaweka reli ya umeme. Ukishafika Morogoro kuja Dodoma kwanza tofauti ile standard gauge na ile reli iliyopo zinatofautiana. Sijui unaanza kupakua hiyo mizigo uweke kwenye ile reli nyingine ile ya zamani na vichwa vile vya … Mimi nadhani kuwe na mpango ambao unakuwa ni wa jumla utachukua muda, lakini mnakuwa na umuhimu wa kusema kwamba tutajenga reli kutoka Dar es Salaam mpaka Kigoma, tutajenga reli kutoka Dar es Salaan mpaka Mwanza.

Mheshimiwa Naibu wa Spika, kitakachokuwepo pale ni kwamba kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro itachukua muda huu; na kutoka Morogoro kwenda Dodoma itachukua muda huu na Dodoma kwenda Mwanza au kwenda Kigoma itachukua muda huu. Na katika muda huo lazima kuwe na mipango thabiti ambayo tunasema kwamba hiyo ni transition period ambayo itakuwa inaeleweka kwa wafanyabiashara na watu wenye viwanda nchini ambapo watakuwa na matarajio yanayoeleweka, na mipango hii ifuatwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, maana kwanza nimeipongeza Serikali kwa namna ya kutafuta revenue.

Hakuna sababu ya kuanza kujenga nusu nusu wakati hujui kinachofuatia na huna mpango wa kupata hela. Ni vyema ukawa umejipanga kwamba nikitoka Dar es Salaam kufika Morogoro nitakuwa nimepata hela za kutoka Morogoro kwenda Dodoma na nikianza kujenga kutoka Morogoro kwenda Dodoma nitakuwa nimepata hela za kutoka Dodoma kwenda Tabora. Tusiwe na mipango ya zima moto. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nisisitize hili la usimamizi wa taasisi na ili watu wengi hatuliwekei umuhimu na hatujui madhara yake. Sielewi kwa nini kwa mfano TCRA ambayo ni shirika ambalo kwa vyovyote vile kulingana na sources za funding yake lazima litajitegemea. Kwa hiyo, pale kinachotakiwa ni kuwa na bodi ambayo ni imara yenye watu wenye kuwaza mawazo mapana. Yale yaliyoko kwenye utaratibu au kwenye sheria TCRA hayo ni ya kawaida, mtu yeyote anaweza akayafanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, these people should think beyond that na tunahitaji watu wanaoweza ku-think beyond that, na hicho ndicho kinatupa tatizo. Watanzania wengi tunajaribu kuwaza leo nitakula nini na jioni nitakula nini. Tukitaka kuendelea ni lazima tuwaze leo tutakula nini, kesho kuna nini, kesho kutwa chakula kitapatikana wapi na wiki ijayo nini tufanye. Haya mawazo ya kuwaza leo hii, halafu kesho hujui, kesho inapofika ndipo unaanza kuwaza, tuondokane nayo.