Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kuchangia kwenye bajeti ya Serikali ya Awamu ya Tano, kwanza kabisa nianze kwa kumpongeza mtumbua majipu Rais wa nchi yetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna ambavyo ameonesha kwa vitendo na kwa kumuenzi Mwalimu Julius Nyerere kwa kauli yake aliyosema kwamba Ikulu ni mahali patakatifu, Ikulu haiwezi kugeuzwa kuwa pango la walanguzi. Ndiyo maana kwa ushupavu kabisa na bila kupepesa macho aliamua kumtumbua Katibu Mkuu Kiongozi ambaye alikuwa Ikulu mahali ambapo ni patakatifu. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Waziri wa Kilimo na Naibu wake wanafanya kazi nzuri, ni wachapakazi hodari na ndiyo maana kukiwa na tatizo kwa wakulima Mheshimiwa Mwigulu huyo na Naibu wake, kukiwa na tatizo kwa wavuvi, Mheshimiwa Mwigulu huyo na Naibu wake, kukiwa na tatizo la mifugo Mheshimiwa Mwigulu huyo na Naibu wake. Mheshimiwa Mwigulu tutaendelea kukupa support katika Bunge hili ili uweze kushughulika na Wizara hii nyeti, Wizara ambayo asilimia 80 ya Watanzania wanaitegemea katika maisha yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kauli mbiu yako inasema kwamba kama tunaitaka mali tutaipata shambani. Mheshimiwa Mwigulu Nchemba hatuwezi tukapata mali shambani kama Wizara yako hautatumbua majipu ambayo yameota sehemu nyeti na Wizara yako ni sehemu nyeti. Kama Kanuni zinaruhusu, kuna majipu nje pale uyaruhusu yaingie humu ndani yaulize kila Mbunge ni mahali gani ya wote kwenye mwili wake, hakuna Mbunge atakayekubali jipu limuote sehemu nyeti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maana gani? Mheshimwia Rais ametumbua jipu la watumishi hewa, Mheshimiwa Mwigulu Wizara ya Kilimo kama Wizara nyeti ina wakulima hewa na wakulima hewa hawa ni jipu ambalo inabidi ulitumbue. Jimboni kwangu na nchi nzima hizi voucher za pembejeo ni jipu la wakulima, wanasajili wakulima hewa, wanasajili wengine wamekufa halafu wanalipa fedha za Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jimboni kwangu kwenye kata moja ya Namhula, voucher za pembejeo zenye thamani ya shilingi 46,320,000 wamewapa wakulima ambao hawapo. Kuna mmoja anaitwa Belita Mnyabwilo yuko Kayenze Mwanza wamemuandika Mwibara kule Mkoa wa Mara kwamba ni mkulima wakati siyo kweli. Kuna Mangasa Mfungo na mdogo wake Ally Mfungo wako Kata nyingine ya Chitengule wameorodheshwa kwenye Kata ya Namhula. Mheshimiwa Mwigulu Nchemba tumbua jipu la wakulima hewa vinginevyo hatutapata mali shambani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jipu lingine la kutumbua Mheshimiwa Mwigulu Nchemba ni la mbegu za pamba zisizoota aina ya quton. Ukiangalia jedwali ukurasa wa 23 wa hotuba ya bajeti, zao la pamba limeshuka mwaka hadi mwaka na sababu kubwa ni mbegu ya quton, mbegu ya kampuni ya mwekezaji fake. Wabunge tumepiga kelele kwenye Bodi ya Pamba wanamkumbatia, hili ni jipu Mheshimiwa Mwigulu Nchemba ikiwezekana ukitoka hapa ukatumbue jipu hili la Kampuni hii ya Quton. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jipu lingine ni la viwanda vya samaki. Wavuvi wanaokwenda kuuza samaki kiwandani, wakifika pale wamefoleni msururu wa magari saa nne, ina bei yake, saa tano bei inashuka, saa sita bei inashuka mpaka kuja kufika saa 12 Wahindi wenye viwanda wanaendelea kushusha bei kwa wavuvi hawa.
Mheshimiwa Mwigulu Nchemba nenda Mwanza pale ukastukize viwanda hivi utaona kilio cha wavuvi wanapunjwa bei, samaki kwa sababu wanaoza wanakosa mahali pa kupeleka. Majipu haya yako sehemu nyeti ya Wizara hii nenda uyatumbue Mheshimiwa Mwigulu Nchemba. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni mbolea. Kama kweli Serikali imekuwa committed kwamba itakuwa Serikali ya viwanda na katika nchi yetu tayari tuna Kiwanda cha Mbolea cha Minjingu, kwa nini Serikali isikitazame kiwanda hiki kwa jicho la huruma kuhakikisha kwamba wanajengewa uwezo wa kuzalisha mbolea kwa wingi ambayo ita-stabilize soko la mbolea na tutaweza kuagiza mbolea kidogo sana kutoka nchi za nje na hatutahitaji dola nyingi za kimarekani. Mheshimiwa Waziri, wewe ni mchapakazi, nenda pale Minjingu angalia matatizo yao, viwanda ambavyo tayari vipo tuanze kuvijengea uwezo hivi kabla hatujajenga vingine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye suala la leseni za uvuvi. Wavuvi hawa wakilipa leseni leo Halmashauri ya Wilaya ya Bunda samaki wanahama wanakimbilia Wilaya ya Busega wavuvi wanawafuata wakifika Busega wanatozwa fedha za leseni nyingine. Samaki wanakimbia wanaenda Ilemela kwa Mheshimiwa Angeline Mabula wanatozwa fedha za leseni kwamba wako Halmashauri nyingine. Samaki wanaogopa upepo siyo rafiki wanakimbilia Ukerewe wakifika kule wanatozwa fedha za leseni. Ndani ya wiki moja, wavuvi hawa maskini wanatozwa leseni kwenye Halmashauri zaidi ya tano na ushahidi tunao.
Mheshimiwa Mwigulu Nchemba hili ni jipu lingine, leseni hizi zinatozwa kitaifa. Kwa nini magari yetu unatoka Songea unakwenda Kagera, unakwenda Lindiā€¦
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa muda wako ndiyo huo.