Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nianze kwanza kumshukuru Mungu kwa kuniruhusu kusimama tena, lakini pia niwashukuru Wenyeviti wote watatu kwa taarifa nzuri za kujenga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye taarifa yetu ya Hali ya Uchumi na Utekelezaji wa Bajeti ya Serikali tulilitaarifu Bunge lako kwamba tumekamilisha majadiliano na taasisi mbalimbali za kifedha ili tuweze kukopa takribani Dola 1,460,000,000 kwa ajili ya kugharamia ujenzi wa reli ya kati na hususani kile kipande cha kutoka Morogoro hadi Makutopora. Naona mdogo wangu alipandisha BP hapa ingawa amenikimbia, anasema sijapata ruhusa ya kwenda kukopa kiasi hicho cha pesa nimeipata wapi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa taarifa ya Bunge ni kwamba tunatafuta fedha hizi kutoka kwenye vyanzo viwili vikubwa, kimoja ni Export Credit Agency (ECA) ambapo tunatarajia tutapata Dola za Kimarekani 990,000,000 lakini zilizobaki takribani Dola 470,000,000 tutakwenda kukopa kwenye vyanzo vya kibiashara na hususani Standard Chartered ambayo imepewa jukumu la kuratibu upatikanaji wa hizo fedha baada ya kukubaliana masharti ya mkopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda wa mkopo wa Export Credit Agency ni miaka 18 wakati kwa mikopo ya kibiashara ni miaka 10 na disbursement ni miaka minne na urejeshaji wake ni kwa miaka 14 kwa upande wa ECA na miaka sita kwa ile mikopo ya kibiashara. Riba unganishi tunaita all cost margin ni asilimia 2.77. Mikopo hii itapatikana ndani ya miaka minne ambayo ni takribani Dola 365 kwa kila mwaka. Kwa hiyo, ule ukomo wa Dola za Marekani milioni 700 ambazo ziko kwenye bajeti hazitavukwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vitu ambavyo nazingatia sana ni Sheria ile ya Mikopo ndiyo inaniongoza kukopa na sheria zake, hakuna kuvuka. Isitoshe kwa mwaka huu fedha Bunge hili liliridhia bilioni 900 kwa ajili ya ujenzi wa awamu ya pili ambayo ni karibu shilingi milioni 800 bila VAT na gharama nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa pia na maneno kwamba kuna trilioni mbili ambazo hazikujumuishwa kwenye Deni la Taifa. Hazikuwekwa huko kwenye kanzidata ya madeni kwa sababu wakati ule tulikuwa bado tunahakiki yale madeni ya mifuko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo napenda kulielezea na hili niliseme na hususani kwa Kamati ile ya Viwanda na Biashara, la Benki Kuu kwamba ile structure yake imepitwa na wakati na sasa tufike mahali ambapo Gavana hawi pia Mwenyekiti wa Bodi. Hili nawasihi sana Waheshimiwa Wabunge tuwe waangalifu sana. Tumeangalia nchi nyingine ulimwenguni takribani asilimia 90 ya nchi ambazo zina structure na majukumu ya Benki Kuu kama ilivyo kwetu hapa wana utaratibu kama huu wa kwetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya msingi kama mnafahamu, Bodi ya Benki Kuu kazi yake ni sera na supervision, kwa hiyo, wao wanapitisha (approve) broad strategies wakati Gavana anasimamia shughuli za kila siku za Benki Kuu na kama mnavyojua sekta ya kibenki ni hypersensitive. Kwa hiyo, ni muhimu sana tukahakikisha kwamba tunaunganisha hizi shughuli za Gavana ili kuhakikisha kwamba Benki inabakia kuwa strong lakini pia Gavana hawezi ku-provide central leadership na independence ya Benki ya Dunia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua unapocheza na exchange rate na interest rate, foreign reserves, money supply, nchi nyingine Gavana akiugua, akipata mafua unaona kule interest rate zinavyoitika. Kwa hiyo, ni muhimu sana tuwe waangalifu tusikimbilie kusema tu-separate hizi nafasi mbili itatugharimu sana, ndiyo uzoefu wa ulimwengu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na suala la utegemezi wa ruzuku ambao umekithiri katika Mashirika ya Umma. Tulipoanzisha haya mashirika shida yetu kubwa ilikuwa ni kutoa huduma kwa jamii kwa urahisi na hususani shughuli zile ambazo hazifanywi na sekta binafsi au kama wanafanya sekta binafsi wanazifanya kwa bei kubwa zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ili tuweze kuhakikisha hizo huduma na hususani upande wa afya, elimu na utafiti zinawafika Watanzania walio wengi, Serikali inatoa ruzuku kwa haya mashirika. Kwa sasa hivi, mashirika ambayo yanapata ruzuku yako takribani 175 ukilinganisha na idadi ya taasisi zote ambazo zipo takribani 269. Kwa hiyo, logic ni ile tu kwamba mashirika haya yanafanya shughuli ambazo private sector haiko kule na kama ipo basi wanafanya kwa gharama kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo napenda kulisemea ni juu ya fees ambazo zinakua charged na Regulatory Authorities. Hili nadhani wote tunakubaliana na mnaona juhudi za Serikali ambazo tumefanya katika hotuba ya bajeti ili tuanze kuzi-rationalize na hii ni continuous process tutaendelea kufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine ni bajeti ya viwanda, limesemwasemwa sana hapa, nataka tu kuomba, taarifa tulizotoa ndizo taarifa rasmi za Serikali. Sasa nimwombe sana Mwenyekiti wa Kamati ya Biashara na Viwanda kama ana taarifa tofauti na takwimu ambazo sisi tumetoa kwenye taarifa rasmi tuliyowasilisha Bungeni, aziwasilishe kwangu kupitia Meza yako Mheshimiwa ili tuweze kuona shida ipo wapi kwenye hizi takwimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda niseme tu la mwisho, yako mengi muda kidogo, hili la conduct ya Sera za Fedha na Sera za Kibajeti, conduct ya monetary na fiscal policy. Ningefurahi sana ningepata muda wa kulieleza vizuri ili tuelewane hususani Mheshimiwa Bashe. Sisi tunavyoliona haziko contradictory kama zinavyowekwa hata kidogo. Tofauti ya kwanza mimi ninayoona ni kwamba ni muhimu kujua hatua ambazo zinachukuliwa hivi sasa baadhi zina matokeo ya mara moja lakini nyingi zinachukua muda ndiyo uweze kuona tofauti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa hivi sasa, tulichokuwa tunafanya tunaita ni Expansionary Monitory Policy. Kwa lugha nyepesi Expansionary Policy ni pale ambapo tunatumia fedha za kibajeti kuongeza zaidi, kuchachua uchumi kwa kuwekeza kwenye miundombinu, tunalipa madai ambayo yamehakikiwa lakini pia kushusha viwango vya kodi kwenye maeneo ambayo tunataka ku-promote kama Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hiyo unakuwa pia na Expansionary Monitory Policy (Sera za Fedha) ambazo Serikali kama ilivyofanya kupunguza statutory minimum reserve requirement lakini saa nyingine inatumia soko lenyewe la fedha (open market operations) lakini pia kujaribu kucheza na riba za aina mbalimbali. Tunavyoziona sisi zipo complimentary tofauti ni muda ambao tunatarajia kwamba tutaona hizo effects tarajiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la muhimu sana, the captains of industry, kama mnasoma magazeti CEO wa NMB ameliweka wazi, CEO wa CRDB ameliweka wazi, nimefanya mazungumzo na zaidi ya benki 12 zote wameweka wazi kwamba wanavyoona wao sekta ya kibenki sasa imeanza kuimarika the worst is over. Sasa tumuamini nani kuliko the captains of industry wenyewe? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la VAT kwenye bidhaa za maziwa na mafuta ghafi, naomba tu niweke tu on record, haya ni mambo ambayo tayari yamepokelewa na yanapelekwa kwenye Kamati za Kitaalam (Think Tank) kwa ajili ya kuchambuliwa. Namwalika Mheshimiwa Mbunge yeyote ambaye atapenda tutatangaza siku ambazo tutakuwa na ile mikutano akitaka aje ashiriki pia yale majadiliano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda niseme tena juu ya upitishaji wa shehena kule bandarini. Nafikiri ni vizuri tupanuke kidogo mawazo, mwenendo wa shehena kwenye bandari zetu hautegemei tu hizi fiscal policies hata kidogo. Ni muhimu kuangalia trends za biashara ulimwenguni zinakwendaje, kwa sababu na bandari zingine ukizitazama the volumes of trade, imports and exports zimekwenda chini siyo kwa Tanzania peke yake. Sasa ukiangalia Tanzania peke yake umefumba macho mno, hebu panua wigo kidogo. Kuna vitu vingi ambavyo inabidi kuviangalia, lazima kuangalia uwezo wa bandari yetu kwa maana ya equipments, lazima pia kuangalia in terms of efficiency hata the way we are organize, kwa maana ya watendaji wa mabenki...

(Hapa Kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.