Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nimefurahi sana nilipoona Wabunge wa CCM wakilia kwamba halmashauri zao hazina fedha. Nimesema hivyo kwa sababu, miezi sita iliyopita wakati tunapitisha bajeti ni Wabunge hao hao ambao walikuwa wanasema bajeti hii ya 2017/2018 ni bajeti ambayo haijawahi kutokea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bajeti mbadala ya Kambi ya Upinzani tulisema wazi kabisa kwamba kwa kitendo cha Serikali kupitia Wizara ya Fedha kunyang’anya vyanzo vya mapato vya halmashauri zetu, vikusanywe na TRA kutoka kwenye halmashauri zetu ni mwanzo wa kuvunja miguu halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni bahati mbaya sana mmetoa muda mchache; kwa sababu ukiangalia hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati anaonesha kama vile fedha za kawaida zilizopelekwa kwenye halmashauri zina-range kwenye asilimia 90; lakini ukipitia hili kabarasha ukiangalia fedha za kawaida, including mishahara yake. Matumizi ya kawaida kwenye fedha ambazo zinaonekana ama zimezidi asilimia 100, ama zimezidi asilimia 150, utakuta ni kwenda kulipa madeni ya wazabuni ya watumishi, ukiwaambia tenganisheni zijulikane za utendaji wa kawaida wa halmashauri na madeni ni zipi, hawasemi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma hiki kitabu, bajeti ya kilimo tunatakiwa tupelekwe bilioni 150 lakini zimepelekwa bilioni 11 nusu ya mwaka. Viwanda tunatakiwa tupeleke bilioni 74 zimepelekwa bilioni saba asilimia tisa. Ndiyo maana mnatupatia dakika saba, tutazungumza nini.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi ya majengo ni mbaya sana pale ambapo Mheshimiwa Waziri unavunja sheria ya bajeti kwa makusudi na nimeleta mabadiliko. Kwa nini nasema hivi; kwanza ufanisi mmeshindwa kukusanya kodi mnatudanganya kwamba mmefanikiwa. Nitakupa mfano wa halmashauri yetu; 2016/2017, Kinondoni tulikusanya bilioni 10 tukiwa na Ubungo. Bilioni 10 a hundred Percent tulikuwa tunapanga kuongeza, mkapata tamaa mkachukua. Mwaka 2016/2017, mmechukua mmeleta bilioni hii, moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi tunaweza kukusanya 10 asilimia 100 mnaleta bilioni moja, hivi huo ni ufanisi? Mwaka 2017/2018, tulikuwa baada ya halmashauri kugawanywa Ubungo ikaenda 2.5, Kinondoni 7.5, tulikuwa tunauwezo wa kukusanya asilimia 100. Wamechukua; sasa hivi miezi sita imepita hata shilingi haijaja. Ninyi mnajua hivi ndivyo vyanzo vyetu vya mapato kisheria, tuliwapa nyie mtukusanyie siyo mchukue mwondoke nazo.

Mheshimiwa nyie mnajua, wamechukua kodi ya mabango. Tulikuwa tuna uwezo wa kukusanya 4.5, a hundred percent billion kwa mwaka uliopita tulikusanya bilioni 3.5 tukaweza kukusanya kwa asilimia 100. Tukasema mwaka huu makadirio yetu tukiongeza tutakuwa na uwezo wa kukusanya mmechukua hamrudishi. Kwa manispaa yangu ninavyozungunza Kinondoni, Iringa, Arusha, Morogoro, hiyo ndiyo mifano. Halafu mnakuja hapa mnasema ufanisi Kinondoni tunashindwa kufanya chochote. Tuna deficit of twelve billion. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Bajeti iko hapa, tulifanya mabadiliko kifungu cha 65 kazi kununua Madiwani tu. Kifungu cha 65 kinasema hivi tulifanya marekebisho mwaka 2016/2017, tukasema, Waziri wa Fedha atashirikiana na Waziri wa TAMISEMI ili wagawane. Wizara inakusanya vipi kupitia TRA halmashauri inakusanya vyanzo vipi vya Property.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2017/2018 mkabadilisha mkamtoa Waziri wetu wa TAMISEMI mkajiweka wenyewe mkasema 65(2) kwamba hizi Property Tax zitakazokuwa collected zitakuwa deposited kwenye Consolidated Fund. Pili 65(2)(a) inasema mgawanyo na msambazo wa zitakazokunywa zinatakiwa zipelekwe halmashauri kutokana na bajeti, ndiyo sheria inavyosema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanajua hawa. Mchakato wa Bajeti huwa unaanzia ngazi ya halmashauri inapitishwa Hazina, inakuja Bungeni. Hizi bajeti za halmashauri tulishazipitisha tokea mwaka jana, inakuwaje leo Mpango eti watatoa kutokana na sisi tutakavyowaambia mahitaji yetu ni nini. Huo siyo utaratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hili tutamtaka Mpango. Tunaomba na Bunge lako Tukufu tuweze kuungana pamoja kwenye azimio ambalo litasema mmeomba mtukusanyie kwa niaba kwa sababu ya ufanisi japokuwa ufanisi hakuna tumekubali; na kwa kuwa tukiwaambia mturudishie tunajua kwa wingi wenu mtakataa lakini tunasema…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzunguzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.